Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutambua siku za wiki katika mawasiliano ya kila siku
  2. kutaja majina ya siku za wiki kwa mfululizo ili kumsaidia kuratibu shughuli za siku,
  3. kuelezea shughuli za siku mbalimbali za wiki ili kujenga stadi ya kuzungumza,
  4. kutumia majina ya siku za wiki kutunga sentensi ili kuimarisha mawasiliano,
  5. kuthamini kila siku ya wiki ili kutilia maanani shughuli za siku husika maishani.

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi atambue siku za wiki yaani:  Jumatatu, Jumanne, Jumatano, Alhamisi, Ijumaa, Jumamosi na  Jumapili kwa kutumia kadi za maneno.
  • Mwanafunzi aweza  kuimba wimbo wa siku za wiki.
  • Mwanafunzi aweza  kukariri mashairi kuhusu siku za wiki.
  • Mwanafunzi ashiriki katika majadiliano ya shughuli za siku za wiki k.m. Jumatatu naenda shule, Ijumaa, Jumamosi au Jumapili nashiriki ibada n.k.
  • Wanafunzi waweza kupanga kadi za majina ya siku za wiki kwa utaratibu wakiwa wawili wawili.

 MASWALI DADISI

  1. Wiki moja ina siku ngapi?
  2. Unaenda shule siku gani?
  3. Unaweza kutaja na kuandika

majina yapi ya siku za wiki kwa mfuatano?

4) Waweza kutumia majina yapi ya siku za wiki katika sentensi?

 Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:

mawasiliano na ushirikiano –  kazi za vikundi  ujuzi wa kidijitali : kuandika kwa vipakatalishi na kusikiliza visa ubunifu: kueleza namna ya kutumia kila siku aliyo nayo.

Uhusiano na masuala mtambuko: stadi za Maisha (uwajibikaji) -kufanya uamuzi wa jinsi ya kutumia siku za wiki uzalendo: kushirikiana katika vikundi.

Uhusiano na Masomo mengine:  Literacy activities, Religious Activities  na

Mathematics Activities

Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

kazi ya vikundi  shughuli za vikundi vya ushirika shuleni michezo nyimbo na mashairi kuhusu siku za wiki.

 Uhusiano na Maadili: 

heshima kwa siku zilizotengewa shughuli za kidini.

Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: 

kusisitiza umuhimu wa shughuli tofauti kwa mfano siku za kwenda shule, siku ya kupumzika na siku ya kwenda maabadini kwa wenzake na miongoni mwa wanajamii.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuchunguza  jinsi anavyoorodhesha siku za wiki na kuzitungia sentensi 
  • kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anaorodhesha siku za wiki kwa haraka na ifaavyo
  • anatumia majina ya siku za wiki katika mawasiliano kwa ubunifu
  • anasimulia kisa kwa ufasaha na ubunifu
  • anajibu maswali ya ufahamu wa hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi. 

 Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anaorodhesha siku za wiki ifaavyo
  • anatumia majina ya siku za wiki katika mawasiliano
  • anasimulia kisa kwa ufasaha
  • anajibu maswali ya ufahamu wa hadithi na masimulizi kwa usahihi. 

 Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika orodhesha siku za wiki ifaavyo
  • ana changamoto katika  kutumia majina ya siku za wiki katika mawasiliano
  • anasimulia baadhi ya visa 
  • anajibu baadhi ya maswali ya ufahamu wa hadithi na masimulizi.

Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto nyingi katika kuorodhesha siku za wiki
  • ana changamoto nyingi katika kutumia majina ya siku za wiki katika mawasiliano
  • Ana changamoto katika kusimulia

visa 

  • Ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu wa hadithi na masimulizi.

CBC Grade 1 Kiswahili Curriculum Designs-4.0 SIKU ZA WIKI-Sub Strand -4.1-Kusikiliza na kuzungumza: Msamiati

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *