MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA
Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-
- kutamka sauti nne za herufi moja katika kuimarisha stadi ya
kuzungumza,
- kutambua sauti za herufi moja zilizofunzwa katika maneno ili kuimarisha stadi ya kuzungumza,
- kutambua majina ya herufi zinazowakilisha sauti lengwa katika kuimarisha stadi ya kusoma,
- kusoma herufi za sauti moja kwa ufasaha ili kuimarisha stadi ya kusoma,
- kusoma maneno kwa kutumia silabi zinazotokana na sauti lengwa kwa ufasaha ili kuimarisha stadi ya kusoma,
- kusoma vifungu vilivyo na maneno yaliyo na sauti lengwa ili kuimarisha stadi ya kusoma,
- kuandika herufi zinazowakilishwa na sauti lengwa ili kuimarisha stadi ya kuandika,
- kuchangamkia kutumia maneno yanayojumuisha sauti zilizofunzwa katika mawasiliano ya kila siku.
MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI
Mwanafunzi aweza kutambua sauti /p/, /f/ na /v/ katika maneno.
- Mwanafunzi asikilize mwalimu akitamka sauti lengwa, kisha atamke pamoja na mwalimu na
mwishowe atamke akiwa peke yake, wawili wawili na kama darasa.
- Mwanafunzi atambue sauti alizosoma katika maneno.
- Mwanafunzi aweza kutumia teknolojia (papaya) kusikiliza matamshi ya sauti lengwa.
- Mwanafunzi atambue herufi zinazowakilisha sauti lengwa kwa kutumia kadi za herufi.
- Mwanafunzi aambatanishe silabi kusoma maneno yanayotokana na sauti lengwa.
- Mwanafunzi atenganishe silabi katika kutambua sehemu mbalimbali za maneno.
- Mwanafunzi aweza kumsikiliza mgeni mwalikwa akitamka sauti lengwa.
- Mwanafunzi asome maneno kwa kutumia silabi au kwa kugawa maneno marefu katika sehemu ndogo ndogo.
- Mwanafunzi aweza kufinyanga maumbo ya herufi.
- Mwanafunzi aandike herufi za sauti alizosoma hewani na vitabuni.
- Wanafunzi wasome hadithi zilizo na maneno yaliyobeba sauti lengwa wakiwa wawili wawili.
- Mwanafunzi aweza kutumia vifaa vya kiteknolojia kama vile tarakilishi, projekta na kipasasauti kusikiliza na kusoma hadithi.
- Mwanafunzi anakili herufi na maneno yanayotokana na sauti alizofunzwa.
- Mwanafunzi aandike maumbo ya herufi na maneno yaliyo na herufi za sauti alizofunzwa.
- Mwanafunzi asikilize imla inayojumuisha maneno yaliyo na herufi za sauti lengwa na kuyaandika.
MASWALI DADISI
1) Ni sauti zipi unazojua kutamka?
- Unajua kusoma herufi na maneno gani?
- Unajua kuandika herufi na maneno gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:
mawasiliano na ushirikiano – wanafunzi wanashiriki katika shughuli za vikundi ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza.
Uhusiano na masuala mtambuko: uraia – haki za watoto -wanafunzi wanahamasishwa kuhusu haki zake.
Uhusiano na Masomo mengine: Environmental Activities
Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:
- kazi ya vikundi
- michezo
- nyimbo na mashairi kuhusu haki za watoto.
Uhusiano na Maadili:
uwajibikaji haki za kijamii heshima.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: kuwahamasisha wengine katika jamii kuhusu haki za watoto.
Mapendekezo ya Tathmini:
- kuchunguza anavyotamka sauti zilizofunzwa
- kuuliza maswali kuhusu haki za watoto
- kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa
- kuchunguza jinsi anavyotumia vizuri na vibaya katika sentensi.
Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini
Kuzidisha Matarajio
Mwanafunzi,
- anatamka sauti lengwa vyema na kwa ukakamavu
- anatambua haki za watoto na kuzitilia maanani katika mawasiliano
- anatumia msamiati wa haki za watoto kwa ubunifu katika sentensi
- anasoma kwa ufasaha
- anatetea haki za watoto kwa ukakamavu
- anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi
- anatumia vivumishi vizuri na vibaya kutunga sentensi ifaavyo na kwa ubunifu wa hali ya juu.
- anaandika kwa hati nadhifu.
Kufikia Matarajio
- Mwanafunzi,
- anatamka sauti lengwa vyema
- anatambua haki za watoto
- anatumia msamiati wa haki za watoto ifaavyo katika sentensi
- anasoma ifaavyo
- anatetea haki za watoto
- anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
- anatumia vivumishi vizuri na vibaya kutunga sentensi ifaavyo anaandika kwa hati bora.
Kukaribia Matarajio
Mwanafunzi,
- ana changamoto katika kutamka baadhi ya sauti lengwa vyema
- anatambua haki za watoto
- ana changamoto katika kutumia baadhi ya msamiati wa haki za watoto kwenye sentensi
- anasoma baadhi ya kazi anazopewa
- anajibu baadhi ya maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
- ana changamoto kiasi katika kutumia vivumishi vizuri na vibaya kutunga sentensi ifaavyo
- anaandika kwa hati zinazosomeka.
Mbali na Matarajio
- Mwanafunzi,
- ana changamoto katika kutamka sauti lengwa
- ana changamoto katika kutambua haki za watoto
- ana changamoto katika kutumia msamiati wa haki za watoto kwenye sentensi
- ana changamoto katika kusoma kazi anazopewa
- ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu kwenye hadithi na masimulizi kwa usahihi
- ana changamoto katika kutumia vivumishi vizuri na vibaya kutunga sentensi ifaavyo
- ana changamoto katika kusoma.