Please Limited time Offer!

CBC Grade 1 Kiswahili Sub strand 2.1

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutambua wenzake darasani kwa majina, jinsia, miaka na gredi ili kuweza kuwaelezea,
  2. kujieleza kwa kurejelea jina, jinsia, miaka na gredi kwa ufasaha katika mawasiliano ya kila siku, 
  3. kutoa muhtasari wa maelezo aliyoyasikiliza katika mazingira yake, 
  4. kudhihirisha umakinifu wa kusikiliza katika mazingira yake, 
  5. kuchangamkia maelezo yake na ya wenzake katika kuimarisha mawasiliano,
  6. kujivunia nafsi yake na wenzake katika miktadha mbalimbali.

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi asikilize maelezo ya wengine.
  • Mwanafunzi aweza kusikiliza maelezo ya wenzake yaliyorekodiwa kwenye simu, kinasa sauti, kipatakalishi n.k.
  • Wanafunzi watoleane maelezo kuwahusu katika vikundi.
  • Wanafunzi wakiwa wawili wawili waulizane maswali na kujibizana k.m. Unaitwaje?
  • Mwanafunzi atoe maelezo yake akizingatia jina, jinsia, umri na gredi mbele ya darasa.
  • Mwanafunzi aeleze maana ya msamiati unaotumiwa kujieleza k.v. umri, miaka,msichana, mvulana, gredi na rafiki.
  • Mwanafunzi atunge sentensi kwa kutumia maneno yanayotumiwa kujieleza na kueleza wenzake.
  • Wanafunzi waweza kujadiliana kuhusu maana na matumizi ya msamiati unaotumiwa k.m. umri, miaka, msichana, mvulana, gredi na rafiki katika vikundi.

MASWALI  DADISI

  1. Wewe ni nani?
  2. Unajua mambo yapi kuhusu mwenzako?
  3. Unapenda kufanya nini?

Umilisi wa kimsingi unaokuzwa: 

Mawasiliano na ushirikiano – Wanatumia lugha faafu katika kujieleza darasani. Vilevile wanashiriki katika kazi ya vikundi Ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza

Uhusiano na masuala mtambuko: Stadi za maisha:  kujitambua na kujithamini kijamii wanapojieleza 

Uhusiano na masomo mengine: English Activities, Literacy and Indigenous Languages na Religious Activities

Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

kazi ya vikundi  shughuli za vikundi vya ushirika shuleni.

 Uhusiano na Maadili: Heshima kwa wengine 

Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: 

kujizatiti kuwajua wenzake shuleni na vijijini kuwafunza wenzake umuhimu wa kuwajua watu katika mazingira yao kwa majina kwa usalama wao.

Mapendekezo ya Tathmini:

kuchunguza  ukakamavu wa mwanafunzi anapojieleza  kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi.

 

 

 

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • ufasaha
  • anaelezea wenzake kwa anajieleza kwa ukakamavu na
  • ukakamavu na ufasaha
  • anasimulia kisa kwa lugha ifaayo na yenye ubunifu
  • anajibu maswali ya ufahamu wa hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi
  • anatoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa kwa ubunifu.

Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anajieleza kwa ufasaha 
  • anaelezea wenzake kwa ufasaha
  • anasimulia kisa kwa lugha ifaayo
  • anajibu maswali ya ufahamu kwa usahihi
  • anatoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa.

 Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anajieleza ifaavyo
  • anaelezea wenzake ifaavyo
  • anasimulia baadhi ya visa 
  • ana changamoto katika  kujibu baadhi maswali kutokana na hadithi
  • ana changamoto katika  kutoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa.

 Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika  kujieleza ifaavyo
  • ana changamoto katika  kuelezea wenzake ifaavyo
  • ana changamoto katika kusimulia

kisa

  • ana changamoto katika kujibu maswali mengi kutokana na hadithi
  • ana changamoto katika kutoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa.

CBC Grade 1 Kiswahili Sub strand 2.1

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *