MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA
Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-
- kusimulia hadithi aliyosikiliza darasani ili kujenga stadi ya kusikiliza,
- kufahamu hadithi aliyosimuliwa ili kupata ujumbe,
- kuonyesha umakinifu wa kusikiliza katika miktadha mbalimbali,
- kuchangamkia hadithi simulizi maishani.
MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI
- Mwanafunzi aweze kuwa makini anaposimuliwa masimulizi kwa kumtazama msemaji na kutofanya lolote anaposikiliza miongni mwa mengine.
- Mwanafunzi asikilize masimulizi kupitia vifaa vya teknolojia k.m. simu, kinasa sauti, kipatakalishi n.k.
- Mwanafunzi aweza kusikiliza mgeni mwalikwa akisimulia masimulizi.
- Wanafunzi waweza kuwekwa katika vikundi na kutoleana muhtasari wa masimulizi yaliyosimuliwa.
- Mwanafunzi aulize na kujibu maswali kutokana na masimulizi.
MASWALI DADISI
- Umewahi kusimuliwa kisa kipi?
- Unatarajiwa kufanya nini unaposimuliwa kisa?
- Unakumbuka nini katika masimulizi uliyosimuliwa?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:
Mawasiliano na ushirikiano – Wanatumia lugha faafu katika kujieleza darasani. Vilevile wanashiriki katika kazi ya vikundi Ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza
Uhusiano na masuala mtambuko: Stadi za maisha: kujitambua na kujithamini kijamii wanapojieleza
Uhusiano na masomo mengine: English Activities, Literacy and Indigenous Languages na Religious Activities
Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:
kazi ya vikundi shughuli za vikundi vya ushirika shuleni.
Uhusiano na Maadili: Heshima kwa wengine
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji:
kujizatiti kuwajua wenzake shuleni na vijijini kuwafunza wenzake umuhimu wa kuwajua watu katika mazingira yao kwa majina kwa usalama wao.
Mapendekezo ya Tathmini:
kuchunguza ukakamavu wa mwanafunzi anapojieleza kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi.
Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini
Kuzidisha Matarajio
Mwanafunzi,
- ufasaha
- anaelezea wenzake kwa anajieleza kwa ukakamavu na
- ukakamavu na ufasaha
- anasimulia kisa kwa lugha ifaayo na yenye ubunifu
- anajibu maswali ya ufahamu wa hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi
- anatoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa kwa ubunifu.
Kufikia Matarajio
Mwanafunzi,
- anajieleza kwa ufasaha
- anaelezea wenzake kwa ufasaha
- anasimulia kisa kwa lugha ifaayo
- anajibu maswali ya ufahamu kwa usahihi
- anatoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa.
Kukaribia Matarajio
Mwanafunzi,
- anajieleza ifaavyo
- anaelezea wenzake ifaavyo
- anasimulia baadhi ya visa
- ana changamoto katika kujibu baadhi maswali kutokana na hadithi
- ana changamoto katika kutoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa.
Mbali na Matarajio
Mwanafunzi,
- ana changamoto katika kujieleza ifaavyo
- ana changamoto katika kuelezea wenzake ifaavyo
- ana changamoto katika kusimulia
kisa
- ana changamoto katika kujibu maswali mengi kutokana na hadithi
- ana changamoto katika kutoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa.