Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutambua msamiati uliyotumika katika hadithi ili kuweza kuutumia katika mawasiliano,
  2. kusikiliza hadithi zikisomwa ili kujenga usikivu,
  3. kufahamu hadithi aliyosomewa darasani ili kupata ujumbe,
  4. kuchangamkia kusikiliza hadithi kila siku.

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi ajadili picha zilizojumuishwa kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi atabiri kitakachotokea kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi athibitishe utabiri wake baada ya kusomewa hadithi.
  • Mwanafunzi aeleze matumizi ya msamiati uliotumika kwenye hadithi.
  • Wanafunzi wajadiliane kuhusu hadithi waliosomewa katika vikundi.
  • Mwanafunzi aweza  kusikiliza hadithi zikisomwa kupitia vifaa vya teknolojia k.v. tarakilishi, projekta n.k.
  • Mwanafunzi aweza kuonyeshwa picha na kadi za msamiati uliotumiwa katika hadithi.

• Mwanafunzi aulize na kujibu maswali kutokana na hadithi.

MASWALI  DADISI

  1. Je, ni hadithi gani ambayo umewahi kusomewa?
  2. Unatarajiwa kufanya nini unaposomewa hadithi?
  3. Unakumbuka nini katika hadithi uliyosomewa?
  4. Unafikiria ni nini kitakachotokea katika hadithi hii?

Umilisi wa kimsingi unaokuzwa: 

Mawasiliano na ushirikiano – Wanatumia lugha faafu katika kujieleza darasani. Vilevile wanashiriki katika kazi ya vikundi Ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza

Uhusiano na masuala mtambuko: Stadi za maisha:  kujitambua na kujithamini kijamii wanapojieleza 

Uhusiano na masomo mengine: English Activities, Literacy and Indigenous Languages na Religious Activities

Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

kazi ya vikundi  shughuli za vikundi vya ushirika shuleni.

 Uhusiano na Maadili: Heshima kwa wengine 

Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: 

kujizatiti kuwajua wenzake shuleni na vijijini kuwafunza wenzake umuhimu wa kuwajua watu katika mazingira yao kwa majina kwa usalama wao.

Mapendekezo ya Tathmini:

kuchunguza  ukakamavu wa mwanafunzi anapojieleza  kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi.

 

 

 

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • ufasaha
  • anaelezea wenzake kwa anajieleza kwa ukakamavu na
  • ukakamavu na ufasaha
  • anasimulia kisa kwa lugha ifaayo na yenye ubunifu
  • anajibu maswali ya ufahamu wa hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi
  • anatoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa kwa ubunifu.

Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anajieleza kwa ufasaha 
  • anaelezea wenzake kwa ufasaha
  • anasimulia kisa kwa lugha ifaayo
  • anajibu maswali ya ufahamu kwa usahihi
  • anatoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa.

 Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anajieleza ifaavyo
  • anaelezea wenzake ifaavyo
  • anasimulia baadhi ya visa 
  • ana changamoto katika  kujibu baadhi maswali kutokana na hadithi
  • ana changamoto katika  kutoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa.

 Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika  kujieleza ifaavyo
  • ana changamoto katika  kuelezea wenzake ifaavyo
  • ana changamoto katika kusimulia

kisa

  • ana changamoto katika kujibu maswali mengi kutokana na hadithi
  • ana changamoto katika kutoa muhtasari wa hadithi aliyosimuliwa.

CBC Grade 1 Kiswahili Curriculum Designs- Sub strand 2.3 Kusoma Hadithi

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *