Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutambua msamiati uliotumika katika hadithi ili kuimarisha ufahamu,

kusikiliza hadithi zikisomwa na  mwalimu zinazojumuisha matukio ya siku za wiki ili kujenga umakinifu,

  • kufahamu hadithi aliyosomewa katika mada ili kupata ujumbe,
  • kuchangamkia kusikiliza hadithi kila siku.

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi ajadili picha zilizojumuishwa kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi atabiri kitakachotokea kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi athibitishe utabiri wake baada ya kusomewa hadithi.
  • Mwanafunzi asikilize hadithi ikisomwa na mwalimu.
  • Mwanafunzi aeleze matumizi ya msamiati uliotumika kwenye hadithi.
  • Wanafunzi waweza kujadiliana kuhusu hadithi waliyosomewa katika vikundi.
  • Mwanafunzi aweza kushirikishwa kusikiliza hadithi kwa kutumia vifaa vya kiteknolojia k.v. tarakilishi, projekta n.k.
  • Mwanafunzi aweza kuonyeshwa picha na kadi za maneno yaliyotumiwa katika hadithi.
  • Mwanafunzi ajibu na aulize maswali kutokana na hadithi.

MASWALI DADISI

  1. Umewahi

kusikiliza hadithi ipi?

  • Unatarajiwa kufanya nini unaposomewa hadithi?
  • Unafikiri ni nini kitakachotokea katika hadithi?
  • Unakumbuka hadithi ipi uliyosomewa?

Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:

mawasiliano na ushirikiano –  kazi za vikundi  ujuzi wa kidijitali : kuandika kwa vipakatalishi na kusikiliza visa ubunifu: kueleza namna ya kutumia kila siku aliyo nayo.

Uhusiano na masuala mtambuko: stadi za Maisha (uwajibikaji) -kufanya uamuzi wa jinsi ya kutumia siku za wiki uzalendo: kushirikiana katika vikundi.

Uhusiano na Masomo mengine:  Literacy activities, Religious Activities  na

Mathematics Activities

Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

kazi ya vikundi  shughuli za vikundi vya ushirika shuleni michezo nyimbo na mashairi kuhusu siku za wiki.

 Uhusiano na Maadili: 

heshima kwa siku zilizotengewa shughuli za kidini.

Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: 

kusisitiza umuhimu wa shughuli tofauti kwa mfano siku za kwenda shule, siku ya kupumzika na siku ya kwenda maabadini kwa wenzake na miongoni mwa wanajamii.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuchunguza  jinsi anavyoorodhesha siku za wiki na kuzitungia sentensi 
  • kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anaorodhesha siku za wiki kwa haraka na ifaavyo
  • anatumia majina ya siku za wiki katika mawasiliano kwa ubunifu
  • anasimulia kisa kwa ufasaha na ubunifu
  • anajibu maswali ya ufahamu wa hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi. 

 Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anaorodhesha siku za wiki ifaavyo
  • anatumia majina ya siku za wiki katika mawasiliano
  • anasimulia kisa kwa ufasaha
  • anajibu maswali ya ufahamu wa hadithi na masimulizi kwa usahihi. 

 Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika orodhesha siku za wiki ifaavyo
  • ana changamoto katika  kutumia majina ya siku za wiki katika mawasiliano
  • anasimulia baadhi ya visa 
  • anajibu baadhi ya maswali ya ufahamu wa hadithi na masimulizi.

Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto nyingi katika kuorodhesha siku za wiki
  • ana changamoto nyingi katika kutumia majina ya siku za wiki katika mawasiliano
  • Ana changamoto katika kusimulia

visa 

  • Ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu wa hadithi na masimulizi.

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *