Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutamka sauti nne za herufi moja ili kuimarisha mazungumzo, 
  2. kutambua sauti za herufi moja zilizofunzwa katika maneno  ili kuimarisha mazungumzo,
  3. kutambua majina ya herufi zinazowakilisha sauti lengwa katika kuimarisha stadi ya kusoma, 
  4. kusoma herufi za sauti moja katika kujenga stadi ya kusoma,
  5. kusoma maneno kwa kutumia

silabi zinazotokana na sauti lengwa katika kujenga stadi ya kusoma,

  • kusoma vifungu vilivyo na maneno yaliyo na sauti lengwa ili kujenga stadi ya

kusoma,  

  • kuandika maumbo ya herufi zinazowakilisha sauti lengwa katika kuimarisha stadi ya kuandika, 
  • kuchangamkia kutumia maneno yanayojumuisha sauti

zilizofunzwa katika mawasiliano ya kila siku.

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi ashirikishwe kutambua sauti /m/, /a/, /u/ na /k/ katika maneno.
  • Mwanafunzi asikilize mwalimu akitamka sauti lengwa, kisha watamke pamoja na mwalimu na mwishowe atamke akiwa peke yake, wawili wawili na katika darasa.
  • Mwanafunzi atumie teknolojia (papaya) kutamkia sauti.
  • Mwanafunzi atambue herufi inayowakilisha sauti lengwa kwa kutumia kadi za herufi.
  • Mwanafunzi aambatanishe silabi kusoma maneno yanayotokana na sauti lengwa.
  • Mwanafunzi atenganishe silabi katika kutambua sehemu mbalimbali za maneno.
  • Wanafunzi waweza kushirikishwa kusikiliza mgeni mwalikwa mwenye umahiri wa kutamka sauti lengwa.
  • Mwanafunzi asome maneno kwa kutumia silabi au kugawa maneno marefu zaidi vipande vipande.
  • Wanafunzi wasome hadithi zilizo na maneno yaliyobeba sauti lengwa kama darasa au wawili wawili.
  • Mwanafunzi asikilize na kusoma hadithi kupitia vifaa vya teknolojia kama vile tarakilishi, projekta n.k. 
  • Mwanafunzi  afinyange na aandike maumbo ya herufi za  sauti alizosoma hewani na vitabuni.
  • Mwanafunzi aandike maneno yaliyo na herufi za sauti alizofunzwa kwa kunakili aliyoandika mwalimu.

MASWALI DADISI

  1. Ni sauti zipi unazojua kutamka?
  2. Unajua kusoma herufi na maneno yapi?
  3. Unajua kuandika herufi na maneno yapi?

 Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:

  • mawasiliano na ushirikiano –  Kujadiliana kuhusu majukumu ya watu wa familia; Kufanya kazi kwa vikundi 
  • hamu ya ujifunzaji: Matumizi ya nafsi ya kwanza wakati uliopo
  • ujuzi wa kidijitali :Kuna mapendekezo ya kutumia vifaa vya kiteknolojia kufunzia
  • ubunifu: Utunzi wa sentensi kwa kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo.

Uhusiano na masuala mtambuko: 

  • uraia: uzalendo: kushirikiana katika vikundi
  • utangamano wa kijamii – mahusiano katika familia.

Uhusiano na masomo mengine: Religious Studies, English Activities na Environmental Activities

 Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

kazi ya vikundi  shughuli za vikundi vya ushirika shuleni michezo.

Mahusiano na Maadili:

mapenzi na heshima katika familia.

Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: 

kutembelea nyumba ya mayatima na kucheza nao kuwaelimisha wengine umuhimu wa familia katika ujenzi wa jamii.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuchunguza  jinsi anavyowatambua watu katika familia yake
  • kuchunguza anavyotamka sauti zilizofunzwa 
  • kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa 
  • kuchunguza jinsi anavyotumia nafsi ya kwanza wakati uliopo katika sentensi.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anawataja watu wa familia zaidi ya aliyofunzwa
  • anatumia majina ya watu wa familia kwa ubunifu katika sentensi
  • anasoma hadithi kwa ufasaha
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi 
  • anatumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi zenye ubunifu
  • anaandika kwa hati nadhifu.

 Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anawataja watu wa familia
  • anatumia majina ya watu wa familia katika sentensi ifaavyo
  • anasoma hadithi
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
  • anatumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi ifaavyo
  • anaandika kwa hati inayosomeka.

Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anawataja watu wa familia
  • anatumia majina ya watu wa

familia katika sentensi 

  • anasoma baadhi ya kazi anazopewa
  • anajibu baadhi maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
  • ana changamoto katika kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi
  • anaandika kwa hati inayosomeka.

 Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • anawataja watu wa familia
  • ana changamoto katika kutumia majina ya watu wa familia katika sentensi 
  • ana changamoto katika kusoma
  • Ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu hadithi na masimulizi kwa usahihi
  • ana changamoto katika kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi
  • ana changamoto katika kuandika.

CBC Grade 1 Kiswahili Curriculum Designs-5.0- FAMILIA-mada ndogo-5.1- Sauti na majina ya herufi za kiswahili

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *