MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA
Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-
- kutambua sauti mbili zinazotamkwa pamoja ili kuimarisha matamshi bora,
- kutamka sauti lengwa ili kuimarisha matamshi bora,
- kusoma silabi za sauti lengwa ili kuimarisha usomaji,
- kusoma maneno kwa kutumia silabi zinazotokana na sauti lengwa ili kuimarisha usomaji,
- kusoma hadithi zilizo na maneno yaliyo na sauti lengwa ili kumsaidia mwanafunzi kutamka sauti husika katika kuimarisha matamshi na usomaji,
- kuandika silabi zinazotokana na sauti lengwa ili kuimarisha uandishi bora,
- kuandika maneno kutokana na silabi zilizofunzwa ili kuimarisha uandishi bora,
- kuchangamkia kutamka sauti lengwa ili kuimarisha mawasiliano.
MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI
- Mwanafunzi atambue sauti mb, nj na ng katika maneno.
- Mwanafunzi amsikilize mwalimu akitamka silabi zinazotokana na sauti lengwa kisha atamke pamoja na mwalimu na baadaye atamke akiwa pekee, wawili na darasa zima. Mifano ya silabi hizi ni: mba, mbe, mbi, nja, nje, nji, nga, nge na ngi.
- Mwanafunzi aweza kutumia teknolojia kama vile papaya, tarakilishi, projekta na kipasasautikipasasauti katika kuimarisha matamshi yake.
- Mwanafunzi aweza kumsikiliza mgeni mwalikwa akitamka sauti lengwa.
- Mwanafunzi atambue sauti alizosikia katika maneno kwa mfano mbuzi, mbuni, Septemba, Disemba, njugu, ngazi na funga
- Mwanafunzi aandike maneno yanayojumuisha sauti lengwa.
- Mwanafunzi asome maneno kwa kuunganisha silabi na kugawa maneno yaliyo marefu zaidi katika sehemu ndogo ndogo.
- Wanafunzi wasome hadithi zilizo na maneno yaliyobeba sauti lengwa darasani au wawili wawili.
- Mwanafunzi asikilize imla ya maneno yenye silabi za sauti lengwa na kuyaandika.
MASWALI DADISI
- Ni sauti zipi unazojua kutamka?
- Unajua kusoma herufi zipi?
- Unajua kuandika herufi na maneno yapi yanayoundwa kutokana na sauti mbili zinazotamkwa pamoja?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:
mawasiliano na ushirikiano – kushirikiana pamoja darasani ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza.
Uhusiano na masuala mtambuko:
elimu ya kudumisha maendeleo: elimu ya maswala ya fedha: kujua kuratibu shughuli za kila siku.
Uhusiano na masomo mengine:
Mathematics Activities, Environmental Activities na English Activities
Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji: kuzingatia ratiba ya shule inayoonyesha shughuli za miezi mbalimbali
Nyimbo na mashairi kuhusu miezi ya mwaka.
Uhusiano na Maadili:
uwajibikaji uzalendo (katika kukumbuka miezi na siku za sherehe za kitaifa).
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: kushiriki katika kuratibu shughuli zinazoendeshwa katika jamii.
Mapendekezo ya Tathmini:
- kuhakiki matamshi ya sauti mbili zinazotamkwa pamoja
- kuchunguza anavyotumia msamiati wa miezi ya mwaka na tarakimu katika mawasiliano
- kuchunguza anavyotumia alama ya kikomo katika mawasiliano
- kuchanganua anavyojibu maswali ya kusema na ya kuandika
- kufuatilia mwandiko wake
kuchunguza anavyotumia lugha katika masimulizi.
Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini
Kuzidisha Matarajio
Mwanafunzi;
- anatamka sauti kwa haraka na ipasavyo
- anasimulia hadithi zinazojumuisha miezi ya mwaka kwa ubunifu
- anasoma hadithi kwa ufasaha na ukakamavu
- anafahamu kwa wepesi hadithi aliyosoma na kusomewa
- anaandika sentensi akitumia kikomo kila siku
- anaandika kisa kwa ubunifu, mtiririko na hati nadhifu na kwa haraka.
Kufikia Matarajio
Mwanafunzi;
- anatamka sauti ipasavyo
- anasimulia hadithi zinazojumuisha miezi ya mwaka
- anasoma hadithi kwa ufasaha
- anafahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
- anaandika sentensi akitumia kikomo
- anaandika kisa kwa mtiririko na hati bora.
Kukaribia Matarajio
Mwanafunzi;
- anatamka baadhi ya sauti ipasavyo
- anasimulia baadhi ya hadithi zinazojumuisha miezi ya mwaka
- anasoma hadithi
- anafahamu baadhi ya hadithi aliyosoma na kusomewa
- anaandika baadhi ya sentensi akitumia kikomo
- anaandika kisa kwa hati zinazosomeka.
Mbali na Matarajio
Mwanafunzi;
- anatamka baadhi ya sauti
- ana changamoto katika kusimulia hadithi zinazojumuisha miezi ya mwaka
- anasoma baadhi ya hadithi japo bila ufasaha ufaao
- ana changamoto katika kufahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
- ana changamoto katika kuandika sentensi akitumia kikomo
- ana changamoto katika kuandika kisa.