Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutaja majina ya ndege mbalimbali ili kuimarisha stadi ya kuzungumza,
  2. kutambua msamiati unaotumiwa katika kutunza ndege ili kuimarisha mawasiliano,
  3. kutumia majina ya ndege katika sentensi sahihi ili kuwezesha mazungumzo,
  4. kutumia msamiati wa kutunza ndege katika sentensi ili kuwezesha mazungumzo,
  5. kusoma maneno na sentensi kuhusu ndege ampendaye ili kujenga usomaji bora,
  6. kuandika maneno na sentensi kuhusu ndege ampendaye ili kujenga uandishi bora,
  7. kuthamini utunzaji wa ndege ampendaye. 

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI 

  • Mwanafunzi atazame picha na kuwatambua ndege tofauti tofauti.
  • Mwanafunzi atunge sentensi sahihi kwa kutumia msamiati kuhusu  ndege.
  • Mwanafunzi atoe maana ya msamiati unaotumiwa katika kutunza ndege.
  • Mwanafunzi achore baadhi ya ndege.
  • Mwanafunzi aweza kutazama video ya utunzaji wa ndege.
  • Mwanafunzi atazame michoro na picha za ndege wa nyumbani wakitunzwa.
  • Mwanafunzi asome maneno na sentensi  katika kadi na chati kuhusu ndege.
  • Mwanafunzi aandike majina na sentensi kuhusu ndege. 

MASWALI DADISI

  1. Ni ndege wepi wanaofugwa?
  2. Unamtunzaje ndege umpendaye?

Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:  mawisiliano na ushirikiano – wanafunzi washiriki katika vikundi na wakiwa wawili wawili ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza hadithi, msamiati na sauti kufikiri kwa kina – kung’amua sifa za ndege ampendaye

Uhusiano na masuala mtambuko: 

elimu ya maendeleo endelevu (masilahi ya wanyama – kujali na kutunza ndege)

Uhusiano na masomo mengine: Environmental Activities na English Activitites.

Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

kushiriki katika vikundi shuleni kama vile chama cha ukulima kuimba na kukariri mashairi kuhusu ndege wa nyumbani.

Uhusiano na Maadili: 

upendo kwa ndege wanaofugwa uwajibikaji katika kutunza ndege.

 Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: kutunza ndege na wanyama.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuchunguza anavyotumia msamiati wa ndege wanaofugwa katika mawasiliano 
  • kuchunguza anavyotumia juu ya na chini ya katika mawasiliano
  • kuchanganua anavyojibu maswali ya kusema na ya kuandika
  • kuchunguza ufahamu wake wa hadithi aliyosoma au kusomewa • kuhakiki anavyosoma na kusimulia hadithi
  • kufuatilia mwandiko wake.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anasikiliza na kusimulia hadithi kwa ukakamavu na ufasaha
  • anasoma maneno, sentensi na hadithi kuhusu ndege ampendaye kwa wepesi na ufasaha
  • anafahamu kwa wepesi hadithi aliyosoma na kusomewa
  • anatumia juu ya na chini ya kutunga sentensi sahihi zenye ubunifu wa hali ya juu
  • anaandika kisa kwa ubunifu, mtiririko, hati nadhifu na kwa haraka.

 Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anasikiliza na kusimulia hadithi kwa ufasaha
  • anasoma maneno, sentensi na hadithi kuhusu ndege ampendaye kwa ufasaha
  • anafahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
  • anatumia juu ya na chini ya kutunga sentensi sahihi
  • anaandika kisa kwa

mtiririko na hati bora.

 Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anasikiliza na kusimulia hadithi
  • anasoma maneno, sentensi na hadithi kuhusu ndege ampendaye 
  • anafahamu baadhi ya hadithi aliyosoma na kusomewa
  • ana changamoto katika kutumia juu ya na chini ya kutunga sentensi sahihi
  • anaandika kisa kwa hati zinazosomeka.

 Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika kusimulia hadithi
  • ana changamoto katika kusoma baadhi ya maneno, sentensi na hadithi kuhusu ndege ampendaye 
  • ana changamoto katika kufahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
  • ana changamoto katika kutumia juu ya na chini ya kutunga sentensi sahihi
  • ana changamoto katika kuandika kisa.

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *