MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA
Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-
- kutambua vyakula vya kiasili ili kuimarisha lishe bora,
- kusoma majina ya vyakula mbalimbali ili kuimarisha stadi ya kusoma,
- kuandika majina ya vyakula katika kuimarisha stadi ya kuandika,
- kutumia majina ya vyakula katika sentensi sahihi,
- kuthamini vyakula vya kiasili katika maisha ya kila siku.
MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI
- Mwanafunzi atambue vyakula mbalimbali vya kiasili kwa kutumia vyakula halisi, picha na michoro ya vyakula kama vile mihogo, viazi, mahindi, maharagwe, mboga na matunda.
- Mwanafunzi atumie msamiati aliyofunzwa kutunga sentensi.
- Mwanafunzi aandike maneno aliyofunzwa.
- Mwanafunzi aweza kupewa kadi za majina ya vyakula vya kiasili asome kwa sauti.
- Wanafunzi waweza kuambatanisha majina ya vyakula halisi au michoro na majina yavyo.
- Wanafunzi waweza kuimba nyimbo na kukariri mashairi kuhusu vyakula vya kiasili.
- Wanafunzi waweza kuandika majina ya vyakula wanavyovijua katika vikundi.
- Wanafunzi waweza kutazama picha za vyakula mbalimbali kupitia kwa vifaa vya kiteknolojia.
MASWALI DADISI
- je, ni vyakula vipi vya kiasili unavyopenda ?
- Vyakula vipi hukuzwa shambani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:
- mawasiliano na ushirikiano – kujadili katika makundi au wawili wawili • hamu ya ujifunzaji: mwanafunzi atajenga msingi wa kujua vyakula zaidi
- ujuzi wa kidijitali –matumizi ya vifaa vya kiteknolojia.
Uhusiano na masuala mtambuko:
elimu ya afya: magonjwa yanayohusiana na vyakula – kuthamini vyakula vya kiasili.
Uhusiano na Masomo mengine:
Health and Nutrition Activities na Environmental Activities
Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:
- kazi ya vikundi
- michezo
- nyimbo na Mashairi kuhusu vyakula vya kiasili.
Uhusiano na Maadili:
uwajibikaji
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji:
kuwahamasisha wengine katika jamii kuhusu umuhimu wa vyakula vya kiasili.
Mapendekezo ya Tathmini:
- kuuliza maswali kuhusu vyakula vya kiasili
- kuchunguza anavyotamka sauti zilizofunzwa
- kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa
- kuchunguza jinsi anavyotumia –angu na -etu katika sentensi.
Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini
Kuzidisha Matarajio
Mwanafunzi,
- anatamka sauti lengwa kwa ufasaha
- anaelezea mifano ya vyakula vya
kiasili
- anatumia msamiati wa vyakula vya kiasili kwa ubunifu katika sentensi
- anasoma kwa ufasaha
- anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi
- anatumia -angu na -etu kutunga sentensi ifaavyo
- anaandika kwa hati nadhifu.
Kufikia Matarajio
Mwanafunzi,
- anatamka sauti lengwa vyema
- anataja mifano ya vyakula vya
kiasili
- anatumia msamiati wa vyakula vya kiasili ifaavyo katika sentensi
- anasoma ifaavyo
- anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
- anatumia -angu na -etu kutunga sentensi ifaavyo
- anaandika kwa hati bora.
. Kukaribia Matarajio
Mwanafunzi,
- ana changamoto katika kutamka baadhi ya sauti lengwa vyema
- anataja mifano ya vyakula vya
kiasili
- ana changamoto katika kutumia baadhi ya msamiati wa vyakula vya kiasili katika sentensi
- anasoma baadhi ya kazi anazopewa
- anajibu baadhi ya maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
- ana changamoto katika kutumia -angu na -etu kutunga sentensi ifaavyo
- ana changamoto katika kusoma.
Mbali na Matarajio
Mwanafunzi,
- ana changamoto katika kutamka sauti lengwa vyema
- ana changamoto katika kutaja mifano ya vyakula vya kiasili
- ana changamoto katika kutumia msamiati wa vyakula vya kiasili katika sentensi
- ana changamoto katika kusoma
- ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi
ana changamoto katika kutumia angu na -etu kutunga sentensi ifaavyo