Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutamka sauti nne za herufi moja katika kuimarisha stadi ya kuzungumza,  
  2. kutambua sauti za herufi moja zilizofunzwa katika maneno

katika kuimarisha stadi ya kuzungumza,

  • kutambua majina ya herufi zinazowakilisha sauti lengwa katika kuimarisha stadi ya kusoma,
  • kusoma herufi za sauti moja katika kuimarisha stadi ya kusoma,
  • kusoma maneno kwa kutumia

silabi zinazotokana na sautilengwa katika kuimarisha stadi ya kusoma,

  • kusoma vifungu vilivyo na maneno yaliyo na sauti lengwa katika kuimarisha stadi ya kusoma,
  • kuandika maumbo ya herufi yanayowakilisha sauti lengwa katika kuimarisha stadi ya kusoma,
  • kuchangamkia kutumia maneno yanayojumuisha sauti lengwa katika mawasiliano ya kila siku.

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi atambue sauti lengwa /s/, /b/, /y/ na /z/ katika maneno.
  • Mwanafunzi asikilize mwalimu akitamka sauti lengwa, kisha atamke pamoja na mwalimu na mwishowe atamke akiwa peke yake, wawili wawili na kama darasa.
  • Mwanafunzi atumie teknolojia (papaya) kutamkia sauti.
  • Mwanafunzi atambue herufi zinazowakilisha sauti lengwa kwa kutumia kadi za herufi.
  • Mwanafunzi aambatanishe silabi kusoma maneno yanayotokana na sauti lengwa.
  • Mwanafunzi atenganishe silabi katika kutambua sehemu mbalimbali za maneno.
  • Wanafunzi waweza kushirikishwa kusikiliza mgeni mwalikwa mwenye umahiri wa kutamka sauti lengwa.
  • Mwanafunzi aweza  kufinyanga maumbo ya herufi inayowakilisha sauti iliyofunzwa.
  • Mwanafunzi aandike maumbo ya herufi za  sauti alizosoma hewani na vitabuni.
  • Mwanafunzi asome maneno kwa kutumia silabi au kwa kugawa maneno marefu katika sehemu ndogo ndogo ili kuyasoma kwa urahisi.
  • Wanafunzi wasome hadithi zilizo na maneno yanayobeba sauti lengwa kama darasa au wawili wawili.
  • Mwanafunzi anaweza kushirikishwa kusikiliza na kusoma hadithi kupitia vifaa vya kiteknolojia kama vile tarakilishi, projekta n.k. 
  • Mwanafunzi ashirikishwe katika kuandika imla ya maneno yaliyo na herufi za sauti alizofunzwa na kuyaandika.

MASWALI DADISI

  1. Ni sauti zipi unazoweza kutamka?
  2. Unajua kusoma herufi  na maneno yapi?
  • Unajua kuandika herufi na maneno?

Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:

  • mawasiliano na ushirikiano –  kujadili katika makundi au wawili wawili

 •          hamu ya ujifunzaji: mwanafunzi atajenga msingi wa kujua vyakula zaidi

  • ujuzi wa kidijitali –matumizi ya vifaa vya kiteknolojia.

Uhusiano na masuala mtambuko: 

elimu ya afya: magonjwa yanayohusiana na vyakula  – kuthamini vyakula vya kiasili.

Uhusiano na Masomo mengine:  

Health and Nutrition Activities na Environmental Activities

 Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

  • kazi ya vikundi 
  • michezo
  • nyimbo na Mashairi kuhusu vyakula vya kiasili.

Uhusiano na Maadili:  

uwajibikaji

 Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: 

kuwahamasisha wengine katika jamii kuhusu umuhimu wa vyakula vya kiasili.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuuliza maswali kuhusu vyakula vya kiasili 
  • kuchunguza anavyotamka sauti zilizofunzwa 
  • kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa 
  • kuchunguza jinsi anavyotumia –angu na -etu katika sentensi.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti lengwa kwa ufasaha
  • anaelezea mifano ya vyakula vya

kiasili

  • anatumia msamiati wa  vyakula vya kiasili kwa ubunifu katika sentensi
  • anasoma kwa ufasaha
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi 
  • anatumia -angu na -etu kutunga sentensi ifaavyo
  • anaandika kwa hati nadhifu.

 Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti lengwa vyema
  • anataja mifano ya vyakula vya

kiasili 

  • anatumia msamiati wa vyakula vya kiasili ifaavyo katika sentensi
  • anasoma ifaavyo
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi 
  • anatumia -angu na -etu kutunga sentensi ifaavyo
  • anaandika kwa hati bora.

 .  Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika kutamka baadhi ya sauti lengwa vyema
  • anataja mifano ya vyakula vya

kiasili

  • ana changamoto katika kutumia baadhi ya msamiati wa  vyakula vya kiasili katika sentensi
  • anasoma baadhi ya kazi anazopewa
  • anajibu baadhi ya maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi 
  • ana changamoto katika kutumia -angu na -etu kutunga sentensi ifaavyo
  • ana changamoto katika kusoma. 

Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika kutamka sauti lengwa vyema
  • ana changamoto katika kutaja mifano ya vyakula vya kiasili 
  • ana changamoto katika kutumia msamiati wa vyakula vya kiasili katika sentensi
  • ana changamoto katika kusoma
  • ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi
  • ana changamoto katika kutumia angu na -etu kutunga sentensi ifaavyo
  • ana changamoto katika kuandika.

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *