Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutambua msamiati uliotumika katika hadithi, 
  2. kusikiliza hadithi zikisomwa na mwalimu zinazohusu familia darasani, 
  3. kusoma hadithi kuhusu familia darasani, 
  4. kufahamu hadithi aliyosomewa kuhusu familia darasani,
  5. kuchangamkia kusikiliza hadithi kila siku.

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

• Mwanafunzi aweza  kujadili picha zilizojumuishwa kwenye hadithi.

  • Mwanafunzi aweza  kutabiri kitakachotokea kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi aweza  kufuatilia hadithi ikisomwa na mwalimu, kisha asome pamoja na mwalimu na baadaye asome akiwa peke yake au wawili wawili.
  • Mwanafunzi aweza  kueleza  maana na matumizi ya msamiati uliotumika kwenye hadithi ukiwemo msamiati wa familia kama vile baba, mama, kaka na dada.
  • Mwanafunzi aweza kusikiliza mwalimu anaposoma hadithi, asome pamoja na mwalimu na kisha asome peke yake, wawili wawili au katika vikundi. 
  • Mwanafunzi asikilize hadithi ya mwalimu au iliyorekodiwa inayojumuisha matumizi ya maneno ya heshima. 
  • Mwanafunzi aweza kutoa muhtasari wa hadithi aliyosoma au aliyosomewa.
  • Wanafunzi waweza kutunga sentensi wakitumia majina ya watu wa familia katika vikundi.
  • Mwanafunzi aweza  kusoma hadithi kwa kutumia jitabu lililowekwa mbele ya darasa. 
  • Mwanafunzi aweza  kuthibitisha utabiri wake baada ya kusomewa hadithi.
  • Wanafunzi waweza kushirikishwa katika kuuliza na kujibu maswali kutokana na hadithi darasani na vilevile kuyaandika kwenye madaftari yao.

MASWALI DADISI

  • Unakumbuka nini katika hadithi uliyosomewa?
  • Unaweza kutabiri kitakachotokea katika hadithi?
  • Unaweza kusoma hadithi?
  • Kwa nini unapenda hadithi?
  • Unakumbuka hadithi gani uliyosoma?

Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:

  • mawasiliano na ushirikiano –  Kujadiliana kuhusu majukumu ya watu wa familia; Kufanya kazi kwa vikundi 
  • hamu ya ujifunzaji: Matumizi ya nafsi ya kwanza wakati uliopo
  • ujuzi wa kidijitali :Kuna mapendekezo ya kutumia vifaa vya kiteknolojia kufunzia
  • ubunifu: Utunzi wa sentensi kwa kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo.

Uhusiano na masuala mtambuko: 

  • uraia: uzalendo: kushirikiana katika vikundi
  • utangamano wa kijamii – mahusiano katika familia.

Uhusiano na masomo mengine: Religious Studies, English Activities na Environmental Activities

 Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

kazi ya vikundi  shughuli za vikundi vya ushirika shuleni michezo.

Mahusiano na Maadili:

mapenzi na heshima katika familia.

Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: 

kutembelea nyumba ya mayatima na kucheza nao kuwaelimisha wengine umuhimu wa familia katika ujenzi wa jamii.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuchunguza  jinsi anavyowatambua watu katika familia yake
  • kuchunguza anavyotamka sauti zilizofunzwa 
  • kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa 
  • kuchunguza jinsi anavyotumia nafsi ya kwanza wakati uliopo katika sentensi.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anawataja watu wa familia zaidi ya aliyofunzwa
  • anatumia majina ya watu wa familia kwa ubunifu katika sentensi
  • anasoma hadithi kwa ufasaha
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi 
  • anatumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi zenye ubunifu
  • anaandika kwa hati nadhifu.

 Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anawataja watu wa familia
  • anatumia majina ya watu wa familia katika sentensi ifaavyo
  • anasoma hadithi
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
  • anatumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi ifaavyo
  • anaandika kwa hati inayosomeka.

Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anawataja watu wa familia
  • anatumia majina ya watu wa

familia katika sentensi 

  • anasoma baadhi ya kazi anazopewa
  • anajibu baadhi maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
  • ana changamoto katika kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi
  • anaandika kwa hati inayosomeka.

 Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • anawataja watu wa familia
  • ana changamoto katika kutumia majina ya watu wa familia katika sentensi 
  • ana changamoto katika kusoma
  • Ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu hadithi na masimulizi kwa usahihi
  • ana changamoto katika kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi
  • ana changamoto katika kuandika.

CBC Grade 1 Kiswahili Curriculum Designs-5.0- FAMILIA-Sub Strand-5.3-Kusoma Hadithi

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *