MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA
Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-
- kutambua maneno na viambishi vinavyotumika kuonyesha nafsi ya kwanza wakati uliopo hali ya umoja na wingi katika sentensi,
- kusoma vifungu vya maneno vinavyoashiria nafsi ya kwanza wakati uliopo hali ya umoja na wingi,
- kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo hali ya umoja na wingi katika sentensi,
- kuandika vifungu vya maneno vinavyoashiria nafsi ya kwanza wakati uliopo hali ya umoja na wingi,
- kufurahia kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo hali ya umoja na wingi katika mawasiliano.
MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI
- Mwanafunzi aweza kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo hali ya umoja na wingi katika mawasiliano.
- Mwanafunzi aweza kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo hali ya umoja na wingi katika sentensi.
- Mwanafunzi aweza kusoma sentensi zinazojumuisha matumizi ya nafsi ya kwanza wakati uliopo hali ya umoja na wingi.
- Mwanafunzi aweza kujaza mapengo kwa kutumia maneno na viambishi vinavyowakilisha nafsi ya kwanza na wakati uliopo kama vile; mimi nina ; sisi tuna.
- Wanafunzi waweza kuigiza nafsi ya kwanza wakati uliopo hali ya umoja na wingi katika vikundi kwa kutumia vifungu kama vile mimi ninaandika-sisi tunaandika, mimi ninasoma- sisi tunasoma baadaye waongozwe kuandika vifungu hivi kwenye madaftari yao.
- Mwanafunzi aweza kupewa zoezi katika tarakilishi ili atumie mbinu ya kuburura majibu sahihi na kutia kapuni.
MASWALI DADISI
- Je, unatumia maneno gani kujirejelea na mkiwa wengi?
- Ukiwa unafanya lolote sasa, utasemaje?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:
- mawasiliano na ushirikiano – Kujadiliana kuhusu majukumu ya watu wa familia; Kufanya kazi kwa vikundi
- hamu ya ujifunzaji: Matumizi ya nafsi ya kwanza wakati uliopo
- ujuzi wa kidijitali :Kuna mapendekezo ya kutumia vifaa vya kiteknolojia kufunzia
- ubunifu: Utunzi wa sentensi kwa kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo.
Uhusiano na masuala mtambuko:
- uraia: uzalendo: kushirikiana katika vikundi
- utangamano wa kijamii – mahusiano katika familia.
Uhusiano na masomo mengine: Religious Studies, English Activities na Environmental Activities
Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:
kazi ya vikundi shughuli za vikundi vya ushirika shuleni michezo.
Mahusiano na Maadili:
mapenzi na heshima katika familia.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji:
kutembelea nyumba ya mayatima na kucheza nao kuwaelimisha wengine umuhimu wa familia katika ujenzi wa jamii.
Mapendekezo ya Tathmini:
- kuchunguza jinsi anavyowatambua watu katika familia yake
- kuchunguza anavyotamka sauti zilizofunzwa
- kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa
- kuchunguza jinsi anavyotumia nafsi ya kwanza wakati uliopo katika sentensi.
Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini
Kuzidisha Matarajio
Mwanafunzi,
- anawataja watu wa familia zaidi ya aliyofunzwa
- anatumia majina ya watu wa familia kwa ubunifu katika sentensi
- anasoma hadithi kwa ufasaha
- anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi
- anatumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi zenye ubunifu
- anaandika kwa hati nadhifu.
Kufikia Matarajio
Mwanafunzi,
- anawataja watu wa familia
- anatumia majina ya watu wa familia katika sentensi ifaavyo
- anasoma hadithi
- anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
- anatumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi ifaavyo
- anaandika kwa hati inayosomeka.
. Kukaribia Matarajio
Mwanafunzi,
- anawataja watu wa familia
- anatumia majina ya watu wa
familia katika sentensi
- anasoma baadhi ya kazi anazopewa
- anajibu baadhi maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
- ana changamoto katika kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi
- anaandika kwa hati inayosomeka.
Mbali na Matarajio
Mwanafunzi,
- anawataja watu wa familia
- ana changamoto katika kutumia majina ya watu wa familia katika sentensi
- ana changamoto katika kusoma
- Ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu hadithi na masimulizi kwa usahihi
- ana changamoto katika kutumia nafsi ya kwanza wakati uliopo kutunga sentensi
- ana changamoto katika kuandika.