Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutambua sehemu za mwili katika mawasiliano,
  2. kutumia majina ya sehemu za mwili katika kutunga sentensi, 
  3. kusoma majina ya sehemu za mwili katika kuimarisha stadi ya kusoma,
  4. kuandika majina ya sehemu za mwili katika kuimarisha stadi ya kuandika,
  5. kuchangamkia utunzaji wa sehemu za mwili katika kuimarisha afya.

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi aambanitishe kadi za maneno na sehemu  za mwili za nje.
  • Mwanafunzi aweza kuonyeshwa video kuhusu sehemu za mwili za nje.
  • Mwanafunzi achore sehemu za mwili za nje.
  • Mwanafunzi afafanue maana ya msamiati wa sehemu za mwili.
  • Mwanafunzi asome hadithi baada ya mwalimu, kisha pamoja na mwalimu na baadaye akiwa peke yake au wawili wawili.
  • Mwanafunzi aweza kushirikishwa katika kuimba  nyimbo na kukariri mashairi yanayohusu sehemu za mwili za nje.
  • Mwanafunzi aandike majina ya sehemu za mwili za nje.
  • Mwanafunzi atunge sentensi kuhusu sehemu za mwili za nje.
  • Mwanafunzi achorewe sehemu za mwili kwenye tarakilishi ili atumie mbinu ya kuburura na kuweka kapuni ili kujazia mapengo.

MASWALI DADISI

  1. Ni sehemu gani ya mwili unayoweza kuchora?
  2. Sehemu tofauti  za mwili za nje zina umuhimu gani?

Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:

mawasiliano na ushirikiano –  kupanga kujadiliana umuhimu wa sehemu za mwili; Kufanya kazi kwa vikundi  hamu ya ujifunzaji: hamu ya kutaka kujua vitu vingine katika umoja na wingi ujuzi wa kidijitali: kuna mapendekezo ya kutumia vifaa vya kiteknolojia kufunzia ubunifu: utunzi wa sentensi katika umoja na wingi.

Uhusiano na masuala mtambuko na Maadili: 

stadi za maisha – kujitambua na kujithamini anapotaja sehemu zake za mwili; kujionea fahari kwa maumbile yake uraia: utangamano wa kijamii – kushirikiana katika vikundi.

Uhusiano na Masomo mengine:  

English Activities, Environmental Activities na Religious Activities  

 Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

kazi ya vikundi  shughuli za vikundi vya ushirika shuleni michezo nyimbo na mashairi.

 Uhusiano na maadili:  Uwajibikaji mapenzi kwa mwili wake.

Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: 

kusisitiza kuhusu utunzaji wa mwili miongoni mwa wenzake kulinda usiri wa mwili wake.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuchunguza  jinsi anavyotambua sehemu mbalimbali za mwili 
  • kuchunguza anavyotamka sauti zilizofunzwa 
  • kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa 
  • kuchunguza jinsi anavyotumia umoja na wingi wa majina katika sentensi.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti lengwa ifaavyo na kwa ukakamavu
  • anaelezea sehemu lengwa za mwili  ifaavyo
  • anatumia majina ya sehemu lengwa za mwili kwa ubunifu katika sentensi
  • anasoma kwa ufasaha
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi 
  • anatumia umoja na wingi wa majina lengwa katika kutunga sentensi ifaavyo kila wakati
  • anaandika kwa hati nadhifu na kwa haraka.

Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti lengwa vyema
  • anataja sehemu lengwa za mwili  ifaavyo
  • anatumia majina ya sehemu lengwa za mwili ifaavyo katika sentensi
  • anasoma ifaavyo
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi 
  • anatumia umoja na wingi wa majina lengwa katika kutunga sentensi ifaavyo
  •  anaandika kwa hati bora.

Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika  kutamka baadhi ya sauti lengwa 
  • anataja sehemu lengwa za mwili  
  • ana changamoto katika kutumia baadhi ya majina ya sehemu lengwa za mwili ifaavyo katika sentensi
  • anasoma baadhi ya kazi anazopewa
  • anajibu baadhi ya maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi 
  • ana changamoto katika kutumia umoja na wingi wa baadhi ya majina lengwa kutunga sentensi anaandika kwa hati zinazosomeka.

Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika kutamka sauti lengwa  
  • ana changamoto katika kutaja baadhi ya sehemu lengwa za mwili 
  • ana changamoto katika kusoma
  • ana changamoto katika kutumia majina ya sehemu lengwa za mwili ifaavyo katika sentensi
  • ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu katikahadithi na masimulizi kwa usahihi
  • ana changamoto katika kutumia umoja na wingi wa majina lengwa kutunga sentensi
  • ana changamoto katika kuandika.

CBC Grade 1 Kiswahili Curriculum Designs-6.0-Sub Strand-6.2 Msamiati

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *