MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA
Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-
- kutamka sauti nne za herufi moja ili kuimarisha mazungumzo,
- kutambua sauti za herufi moja zilizofunzwa katika kujenga stadi ya kusikiliza,
- kutambua majina ya herufi zinazowakilisha sauti lengwa katika kujenga stadi ya kusikiliza,
- kusoma herufi za sauti moja katika kujenga stadi ya kusoma,
- kusoma maneno kwa kutumia silabi zinazotokana na sauti lengwa katika kujenga stadi ya kusoma,
- kusoma vifungu vilivyo na maneno yaliyo na sauti lengwa katika kujenga stadi ya kusoma,
- kuandika herufi zinazowakilishwa na sauti lengwa katika kujenga stadi ya kuandika,
- kuchangamkia kutumia maneno yanayojumuisha sauti zilizofunzwa katika mawasiliano ya kila siku.
MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI
- Mwanafunzi atamke sauti /g/, /d/, /j/, na /r/ katika maneno.
- Mwanafunzi asikilize mwalimu akitamka sauti lengwa, kisha atamke pamoja na mwalimu na mwishowe atamke akiwa peke yake, wawili wawili na kama darasa.
- Mwanafunzi atambue sauti alizosoma katika maneno.
- Mwanafunzi aweza kutumia teknolojia (papaya) kusikiliza matamshi ya sauti lengwa.
- Mwanafunzi atambue herufi zinazowakilisha sauti lengwa kwa kutumia kadi za herufi.
- Mwanafunzi aambatanishe silabi kusoma maneno yanayotokana na sauti lengwa.
- Mwanafunzi atenganishe silabi katika kutambua sehemu mbalimbali za maneno.
- Mwanafunzi aweza kumsikiliza mgeni mwalikwa akitamka sauti lengwa.
- Mwanafunzi asome maneno kwa kutumia silabi au kwa kuyagawa maneno marefu katika sehemu fupi fupi.
- Mwanafunzi aandike herufi za sauti alizosoma hewani na vitabuni.
- Mwanafunzi aweza kufinyanga maumbo ya herufi.
- Wanafunzi wasome hadithi zilizo na maneno yaliyobeba sauti lengwa wakiwa wawili wawili.
- Mwanafunzi aweza kutumia vifaa vya kiteknolojia kama vile tarakilishi, projekta na kipasasauti kusikiliza na kusoma hadithi.
- Mwanafunzi anakili herufi na maneno yanayotokana na sauti alizofunzwa.
- Mwanafunzi aandike maumbo ya herufi na maneno yaliyo na herufi za sauti alizofunzwa.
- Mwanafunzi asikilize imla inayojumuisha maneno yaliyo na herufi za sauti lengwa na kuyaandika.
MASWALI DADISI
- Je, ni sauti zipi unazojua kutamka?
- Unajua kusoma herufi na maneno gani?
- Unajua kuandika herufi na maneno gani?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:
mawasiliano na ushirikiano – wanafunzi wanashiriki katika vikundi ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza kujiamini/kujithamini – kuigiza na kusimulia.
Uhusiano na masuala mtambuko na maadili:
uraia – utangamano wa kijamii wanafunzi watangamane na kufanya kazi pamoja.
Uhusiano na masomo mengine: English Activities, Literacy and Indigenous Languages Activities na Environmental activities.
Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:
- kazi ya vikundi
- michezo
- nyimbo na mashairi kuhusu shule.
Uhusiano na Maadili:
Uwajibikaji.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: kuwahamasisha wengine katika jamii kuhusu umuhimu wa shule.
Mapendekezo ya Tathmini:
- kuuliza maswali kuhusu shuleni
- kuchunguza anavyotamka sauti zilizofunzwa
- kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa
- kuchunguza jinsi anavyotumia –ako na -enu katika sentensi.
Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini
Kuzidisha Matarajio
Mwanafunzi,
- anatamka sauti lengwa kwa ukakamavu na ufasaha
- anatumia msamiati wa shuleni katika sentensi ifaavyo na kwa ubunifu
- anasoma kwa ufasaha
- anatumia nambari kumi na moja hadi hamsini kwa ubunifu katika sentensi
- anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi
- anatumia -ako na -enu kutunga sentensi ifaavyo kila wakati
- anaandika kwa hati nadhifu na kwa haraka.
Kufikia Matarajio
Mwanafunzi,
- anatamka sauti lengwa vyema
- anatumia msamiati wa shuleni ifaavyo katika sentensi
- anasoma ifaavyo
- anatumia nambari kumi na moja hadi hamsini ifaavyo katika sentensi
- anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
- anatumia -ako na -enu kutunga sentensi ifaavyo
- anaandika kwa hati zinazosomeka.
.
Kukaribia Matarajio
Mwanafunzi,
- ana changamoto katika kutamka baadhi ya sauti lengwa vyema
- ana changamoto katika kutumia baadhi ya msamiati wa shuleni katika sentensi
- ana changamoto kiasi katika kusoma
- ana changamoto katika kutumia baadhi ya nambari kutoka kumi na moja hadi hamsini kwenye sentensi
- anajibu baadhi ya maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
- ana changamoto katika kutumia -ako na -enu kutunga sentensi ifaavyo
- anaandika kwa hati zinazosomeka.
Mbali na Matarajio
Mwanafunzi,
- ana changamoto katika kutamka sauti lengwa
- ana changamoto katika kutumia msamiati wa shuleni kwenye sentensi
- ana changamoto nyingi katika kusoma
- ana changamoto katika kutumia majina ya nambari kutoka kumi na moja hadi hamsini kwenye sentensi
- ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi
- ana changamoto katika kutumia ako na -enu kutunga sentensi ifaavyo
- ana changamoto katika kuandika.