Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutambua matumizi yafaayo ya vizuri na vibaya katika mawasiliano
  2. kutumia vizuri na vibaya katika sentensi sahihi ili kuimarisha mawasiliano
  3. kusoma sentensi  zinazojumuisha vizuri na vibaya ili kuimarisha usomaji bora
  4. kuandika sentensi kwa kujumuisha vizuri na vibaya ili kuimarisha uandishi mwafaka

e) kuchangamkia matumizi ya vizuri na vibaya katika kuimarisha mawasiliano.

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi aweza kujaza mapengo kwa kutumia vizuri na vibaya.  
  • Mwanafunzi aweza kubainisha matumizi ya vielezi lengwa kwa kutumia vifaa vya kiteknolojia.
  • Mwanafunzi arejelee vitendo mbalimbali kwa kutumia vizuri na vibaya k.m Mtoto amesoma vizuri.
  • Mwanafunzi aandike sentensi zinazojumuisha vizuri na vibaya.

MASWALI DADISI

  1. Unatumia maneno yapi kuelezea vile mtu alivyofanya jambo?

Umilisi wa kimsingi unaokuzwa: 

mawasiliano na ushirikiano – wanafunzi wanashiriki katika shughuli za vikundi ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza.

Uhusiano na masuala mtambuko:  uraia – haki za watoto -wanafunzi wanahamasishwa kuhusu haki zake.                   

Uhusiano na Masomo mengine: Environmental Activities

 Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

  • kazi ya vikundi 
  • michezo
  • nyimbo na mashairi kuhusu haki za watoto.

 Uhusiano na Maadili:  

uwajibikaji haki za kijamii heshima.

Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji:  kuwahamasisha wengine katika jamii kuhusu haki za watoto.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuchunguza anavyotamka sauti zilizofunzwa
  • kuuliza maswali kuhusu haki za watoto 
  • kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa
  • kuchunguza jinsi anavyotumia vizuri na vibaya katika sentensi.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti lengwa vyema na kwa ukakamavu
  • anatambua haki za watoto na kuzitilia maanani katika mawasiliano 
  • anatumia msamiati wa haki za watoto kwa ubunifu katika sentensi
  • anasoma kwa ufasaha
  • anatetea haki za watoto kwa ukakamavu
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi 
  • anatumia vivumishi vizuri na vibaya kutunga sentensi ifaavyo na kwa ubunifu wa hali ya juu.
  • anaandika kwa hati nadhifu.

 Kufikia Matarajio

  • Mwanafunzi,
  • anatamka sauti lengwa vyema
  • anatambua haki za watoto 
  • anatumia msamiati wa haki za watoto ifaavyo katika sentensi
  • anasoma ifaavyo
  • anatetea haki za watoto
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
  • anatumia vivumishi vizuri na vibaya kutunga sentensi ifaavyo anaandika kwa hati bora.

Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika kutamka baadhi ya sauti lengwa vyema
  • anatambua haki za watoto 
  • ana changamoto katika  kutumia baadhi ya msamiati wa haki za watoto kwenye sentensi
  • anasoma baadhi ya kazi anazopewa
  • anajibu baadhi ya maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
  • ana changamoto  kiasi katika kutumia vivumishi vizuri na vibaya kutunga sentensi ifaavyo
  • anaandika kwa hati zinazosomeka.

Mbali na Matarajio

  • Mwanafunzi,
  • ana changamoto katika  kutamka sauti lengwa
  • ana changamoto katika kutambua haki za watoto 
  • ana changamoto katika  kutumia msamiati wa haki za watoto kwenye sentensi
  • ana changamoto katika kusoma kazi anazopewa
  • ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu kwenye  hadithi na masimulizi kwa usahihi
  • ana changamoto katika kutumia  vivumishi vizuri na vibaya kutunga sentensi ifaavyo
  • ana changamoto katika kusoma.

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *