Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutambua baadhi ya majina ya vyombo vya usafiri katika kuimarisha mawasiliano,
  2. kusoma majina ya vyombo vya usafiri na msamiati mwingine wa usafiri katika sentensi ili kuimarisha usomaji bora,
  3. kutumia msamiati wa usafiri kutungia sentensi katika kuimarisha stadi ya kuzungumza na kuandika, 
  4. kuandika majina ya vyombo vya usafiri na msamiati mwingine wa usafiri ili kuimarisha stadi ya kuandika,
  5. kuthamini vyombo vya usafiri katika maisha ya kila siku. 

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi atunge sentensi sahihi akitumia msamiati wa vyombo vya usafiri k.v. matatu, basi, lori, pikipiki, garimoshi, gari dogo,  ndege na meli.
  • Mwanafunzi atoe maana ya msamiati unaohusu usafiri.
  • Mwanafunzi aweza kutazama michoro na picha zinazolenga usafiri.
  • Mwanafunzi achore baadhi ya vyombo vya usafiri na kuvitambua kwa majina.
  • Mwanafunzi aweza kutazama video kuhusu  shughuli za usafiri.
  • Wanafunzi wajadiliane kuhusu umuhimu wa vyombo vya usafiri.

MASWALI DADISI

  1. Umewahi kutumia chombo kipi cha  kusafiria?
  2. Unajua vyombo gani vingine vya usafiri?
  3. Je, ni maneno gani  yanayotumiwa usafiri?

Umilisi wa kimsingi unaokuzwa: 

mawasiliano na ushirikiano – wanafunzi wanashiriki katika kazi za vikundi  ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza hamu ya kujifunza: mwanafunzi atapata hamu ya kutaka kutumia vipengee vilivyofunzwa vya sarufi kwenye mawasiliano ubunifu – mwanafunzi anatumia ubunifu katika kutunga sentensi na masimulizi.

Uhusiano na masuala Mtambuko: 

elimu ya maendeleo endelevu- usalama katika usafiri –wanashughulikia vyombo vya usafiri.  

Uhusiano na Masomo Mengine: 

Environmental Activities na English Activities                                                                               

Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

  • kazi ya vikundi 
  • michezo
  • mashairi na nyimbo kuhusu usafiri 

 Uhusiano na Maadili:  

uwajibikaji  heshima.

 Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji:  kuwahamasisha wengine kuhusu usalama barabarani.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuchunguza anavyotamka sauti zilizofunzwa
  • kuuliza maswali kuhusu vyombo vya usafiri 
  • kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa 
  • kuchunguza jinsi anavyotumia herufi kubwa kuakifisha maneno na sentensi.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti lengwa kwa ufasaha
  • anataja majina ya vyombo vya usafiri kwa wepesi 
  • anatumia msamiati wa usafiri kwa ubunifu katika sentensi
  • anasoma kwa ufasaha.
  • anafahamu kwa urahisi hadithi aliyosimuliwa, aliyosoma na kusomewa
  • anatumia herufi kubwa ipasavyo katika kuakifisha maneno na sentensi kwa wakati
  • anaandika kwa hati nadhifu na kwa haraka.

 Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti lengwa vyema
  • anataja majina ya vyombo vya

usafiri 

  • anatumia msamiati wa usafiri ifaavyo katika sentensi
  • anasoma ifaavyo
  • anafahamu hadithi aliyosimuliwa,  aliyosoma na kusomewa
  • anatumia herufi kubwa ipasavyo katika kuakifisha maneno na sentensi
  • anaandika kwa hati bora.

 Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika kutamka baadhi ya sauti lengwa vyema
  • anataja baadhi ya majina ya vyombo vya usafiri 
  • ana changamoto katika kutumia baadhi ya msamiati wa usafiri kwenye sentensi
  • anasoma baadhi ya kazi anazopewa
  • anafahamu  baadhi ya hadithi alizosimuliwa, aliyosoma au kusomewa
  • ana changamoto kiasi katika kuakifisha maneno na sentensi kwa kutumia herufi kubwa
  • anaandika kwa hati zinazosomeka.

Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika kutamka sauti lengwa 
  • ana changamoto katika kutaja baadhi ya majina ya vyombo vya usafiri 
  • ana changamoto katika kutumia msamiati wa usafiri kwenye sentensi
  • ana changamoto katika kusoma
  • ana changamoto katika kufahamu hadithi aliyosimuliwa, aliyosoma au kusomewa
  • ana changamoto  katika kuakifisha maneno na sentensi kwa kutumia herufi kubwa
  • ana changamoto katika kuandika.

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *