Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:- 

  1. kutambua picha zinazoonyesha usalama katika mazingira mbalimbali ili kurahisisha ufahamu,
  2. kutambua maneno yanayohusiana na usalama ili kuyatumia katika mawasiliano,
  3. kusikiliza hadithi za mwalimu kuhusu usalama ili kuimarisha ufahamu,
  4. kusoma hadithi kuhusu usalama ili kujenga usikivu,
  5. kufahamu hadithi aliyoisoma na aliyosomewa kuhusu usalama ili kupata ujumbe, 
  6. kuthamini umuhimu wa usalama katika maisha ya kila siku. 

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI 

  • Mwanafunzi ajadili picha zilizojumuishwa kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi atabiri kitakachotokea kwenye hadithi
  • Mwanafunzi afahamu matumizi ya msamiati uliotumika kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi ashiriki kusoma kama darasa, wakiwa wawili wawili na baadaye asome peke yake.
  • Wanafunzi wasomeana hadithi wakiwa wawili wawili au katika vikundi.
  • Mwanafunzi aweza kusikiliza hadithi husika ikisomwa kupitia kinasasauti.
  • Mwanafunzi aweza kutazama video ya mtu mzima au mtoto akisoma hadithi husika kwa ufasaha kisha aige usomi huo
  • Mwanafunzi athibitishe utabiri wake baada ya kusoma hadithi.
  • Mwanafunzi aweza kusimulia hadithi kutokana na picha alizopewa kuhusu usalama.
  • Mwanafunzi atoe muhtasari wa hadithi aliyosoma au kusomewa.
  • Mwanafunzi ajibu na kuuliza maswali kutokana na hadithi.

MASWALI DADISI

  1. Je, usalama unahusu nini?
  2. Ukosefu wa salama husababishwa na nini?
  3. Unapokosa usalama unafaa kufanya nini?

 Umilisi wa kimsingi unaokuzwa: 

mawisiliano na ushirikiano – wanafunzi washiriki katika vikundi ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza ubunifu – unadhihirishwa na usimulizi na utungaji wa sentensi.

Uhusiano na masuala mtambuko: 

Elimu ya maendeleo endelevu: elimu ya usalama – kupitia kwa kutambua umuhimu na mbinu za kujilinda na hali zinazohatarisha usalama

Stadi za maisha – mbinu za kujilinda dhidi ya tisho kwa usalama wake.

Uhusiano na masomo mengine: Environmental Activities; Hygiene and Nutrition na English Activities.

Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

Kushiriki katika kuimba nyimbo na kukariri mashairi kuhusu usalama katika tamasha mbalimbali.

Uhusiano na Maadili: 

uwajibikaji -kuwa na msimamo thabiti katika uamuzi wake haki za kijamii- kufuata haki zake anapodhulumiwa.

 Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: kusaidia kuhamasisha jamii kuhusu usalama kushiriki katika kutetea haki za kijamii.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuchunguza anavyotumia msamiati wa usalama katika mawasiliano 
  • kuchunguza anavyotumia vinyume vya vitendo katika mawasiliano
  • kuchanganua anavyojibu maswali ya kusema na ya kuandika
  • kuchunguza ufahamu wake wa hadithi aliyosoma au kusomewa • kuhakiki anavyosoma na kusimulia hadithi
  • kufuatilia mwandiko wake.
  •  

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatambua na kutumia mbinu mbalimbali za kujiepusha na hali zinazoweza kuhatarisha usalama wake
  • anatumia maneno ya maagano
  • ifaavyo kila wakati
  • anasimulia kisa alichokishuhudia kuhusu usalama kwa ubunifu na ufasaha
  • anasoma maneno, sentensi na hadithi  kwa ufasaha na ukakamavu
  •  anaandika vinyume vya vitendo kwa usahihi
  •  anaandika kisa kwa ubunifu, mtiririko, kwa hati nadhifu na kwa kasi ifaayo. 

Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatambua mbinu mbalimbali za kujiepusha na hali zinazoweza kuhatarisha usalama wake
  • anatumia maneno ya maagano ifaavyo
  • anasimulia kisa alichokishuhudia kuhusu usalama kwa ufasaha
  • anasoma maneno, sentensi na hadithi  kwa ufasaha
  • anaandika vinyume vya vitendo kwa usahihi
  • anaandika kisa kwa mtiririko na hati bora. 

Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

•             anatambua mbinu mbalimbali za kujiepusha na hali zinazoweza kuhatarisha usalama wake

•             anatumia maneno ya maagano ifaavyo

•             anaelezea kuhusu kisa alichoshuhudia bila mtiririko wenye mantiki

•             anasoma maneno, sentensi na baadhi ya hadithi  kwa ufasaha

 •            ana changamoto katika kuandika vinyume vya baadhi ya vitendo kwa usahihi

•             anaandika kisa kwa hati zinazosomeka.

Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

•             ana changamoto katika kutambua mbinu mbalimbali za kujiepusha na hali zinazoweza kuhatarisha usalama wake

•             ana changamoto katika kutumia baadhi ya maneno ya maagano kwenye mawasiliano

•             ana changamoto katika kusimulia kisa alichokishuhudia kuhusu usalama

•             ana changamoto katika kusoma maneno, sentensi na hadithi  kwa ufasaha

•             ana changamoto katika kuandika vinyume vya vitendo kwa usahihi

•             ana changamoto katika kuandika kisa.

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *