Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kusikiliza kwa makini masimulizi kuhusu shambani katika kujenga usikivu
  2. kutaja majina ya vifa vinavyotumika shambani ili kuimarisha stadi ya kuzungumza
  3. kuelezea vifaa vinavyotumika shambani ili kuimarisha stadi ya kuzungumza
  4. kuelezea shughuli zinazofanyika shambani ili kuimarisha stadi ya kuzungumza
  5. kutambua matumizi ya vifaa vinavyotumika shambani ili kuimarisha stadi ya kuzungumza

f) kuthamini umuhimu wa vifaa vinavyotumika shambani.

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi kusimulie visa kuhusu shambani.
  • Mwanafunzi ashiriki katika mjadala kuhusu  vifaa vinavyotumika shambani kama vile;  jembe, shoka, upanga, kifyekeo, plau, trekta, lima, fyeka na panda akionyeshwa vifaa halisi, picha au michoro.
  • Mwanafunzi aelezee umuhimu wa  vifaa vinavyotumika shambani.
  • Mwanafunzi aweza kushirikishwa katika nyimbo au mashairi  kuhusu vifaa vinavyotumika shambani.
  • Mwanafunzi aweza kushirikishwa katika kuigiza vitendo vinavyofanywa shambani kama vile kulima, kufyeka na kupanda.
  • Mwanafunzi aweza kutazama video inayoonyesha jinsi vifaa mbalimbali vinavyotumika shambani
  • Mwanafunzi anaweza kutumia tarakilishi kutambua vifaa mbalimbali kwa majina vilivyo.

MASWALI DADISI

  1. Je, ni vifaa vipi hutumika  shambani?
  2. Ni shughuli zipi zinazofanyika shambani?

 Umilisi wa kimsingi unaokuzwa: 

mawasiliano na ushirikiano – Wanatumia lugha faafu darasani. Vilevile wanashirikiana katika kazi ya vikundi. ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza.

ubunifu: mwanafunzi napoandika au kusimulia kisa kufikiria kwa kina na kutatua matatizo – mwanafunzi anapojibu maswali ambayo majibu yake hayapatikani moja kwa moja kutoka kwenye kisa  hamu ya ujifuzaji – mwanafunzi atapata hamu ya kutaka kujua matumizi ya vifaa vya shambani.

Uhusiano na masuala mtambuko: 

elimu ya maendeleo endelevu: athari za majanga – kujua athari za vifaa vya shambani uraia : kuthamini kilimo katika kukuza uchumi wa nchi.

Uhusiano na masomo mengine: Environmental activities

Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

kushiriki katika vikundi vya ushirika shuleni vinavyohusu ukulima kushiriki katika kilimo shuleni. 

Uhusiano na Maadili:                                       

uwajibikaji katika kutunza vifaa vya shambani kutunza vifaa vya shambani.

 Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: kushiriki katika ukulima nyumbani

Kuwahamasisha wengine wa rika lake kuhusu umuhimu wa kilimo.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuhakiki matamshi ya sauti mbili zinazotamkwa pamoja
  • kuchunguza anavyotumia msamiati wa shambani katika mawasiliano
  • kuchunguza anavyotumia nafsi ya tatu wakati ujao katika mawasiliano • kuchanganua anavyojibu maswali ya kusema na ya kuandika
  • kufuatilia mwandiko wake.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti lengwa kwa ufasaha
  • anasimulia shughuli zinazofanyika shambani kwa ubunifu
  • anasoma hadithi kwa ufasaha na ukakamavu
  • anafahamu kwa urahisi hadithi aliyosoma na kusomewa
  • anaandika kisa kifupi kwa hati nadhifu na ubunifu
  • anatunga sentensi sahihi akizingatia nafsi ya tatu wakati ujao katika umoja na wingi kila wakati.

Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti ipasavyo
  • anasimulia shughuli zinazofanyika shambani
  • anasoma hadithi kwa ufasaha.
  • anafahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
  • anaandika kisa kifupi kwa hati bora
  • anatunga sentensi sahihi akizingatia nafsi ya tatu wakati ujao katika umoja na wingi.

Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka baadhi ya sauti ipasavyo
  • anasimulia baadhi ya shughuli za shambani
  • anasoma hadithi kwa ufasaha
  • ana chamgamoto katika kufahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
  • anajaribu kuandika kisa kwa hati inayosomeka
  • ana changamoto katika kutunga sentensi sahihi akizingatia nafsi ya tatu wakati ujao katika umoja na wingi.

Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika kutamka sauti alizofunzwa 
  • ana changamoto katika kusimulia shughuli za shambani
  • ana changamoto katika kusoma hadithi  
  • ana chamgamoto katika kufahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
  • ana changamoto katika kuandika kisa
  • ana changamoto katika kutunga sentensi sahihi akizingatia nafsi ya tatu wakati ujao katika umoja na wingi

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *