Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutambua picha za vifaa vinavyotumika shambani ili

kuimarisha ufahamu wa hadithi,

  • kusoma hadithi za picha zinazohusu shamba ili kujenga usomaji bora, 
  • kusikiliza hadithi zikisomwa na mwalimu kuhusu vifaa  vinavyotumika shambani ili kujenga usikivu,
  • kufahamu hadithi aliyoisoma na aliyosomewa kuhusu shambani ili kupata ujumbe,
  • kuchangamkia kusoma hadithi za vifaa vinavyotumika shambani ili kuendeleza stadi ya usomaji.

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi ajadili picha zilizojumuishwa kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi atabiri kitakachotokea kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi afahamu matumizi ya msamiati uliotumika kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi asome na wengine darasani, wakiwa wawili na baadaye asome peke yake.
  • Wanafunzi waweza kusomeana hadithi wakiwa wawili wawili au katika vikundi.
  • Mwanafunzi aweza kusoma hadithi kwa kutumia vifaa vya kiteknolojia k.m. tarakilishi na projekta.
  • Mwanafunzi aweza  kusoma hadithi kwa kutumia jitabu lililowekwa mbele ya darasa. 
  • Mwanafunzi athibitishe utabiri wake baada ya kusoma hadithi.
  • Mwanafunzi atoe muhtasari wa hadithi aliyosoma.
  • Mwanafunzi ajibu na kuuliza maswali kuhusu hadithi aliyosoma.

MASWALI DADISI

  1. Unaona nini katika picha?
  2. Ni nini kitakachotendeka katika hadithi?
  3. Ni vifaa vipi vimetajwa katika hadithi?

Umilisi wa kimsingi unaokuzwa: 

mawasiliano na ushirikiano – Wanatumia lugha faafu darasani. Vilevile wanashirikiana katika kazi ya vikundi. ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza.

ubunifu: mwanafunzi napoandika au kusimulia kisa kufikiria kwa kina na kutatua matatizo – mwanafunzi anapojibu maswali ambayo majibu yake hayapatikani moja kwa moja kutoka kwenye kisa  hamu ya ujifuzaji – mwanafunzi atapata hamu ya kutaka kujua matumizi ya vifaa vya shambani.

Uhusiano na masuala mtambuko: 

elimu ya maendeleo endelevu: athari za majanga – kujua athari za vifaa vya shambani uraia : kuthamini kilimo katika kukuza uchumi wa nchi.

Uhusiano na masomo mengine: Environmental activities

Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

kushiriki katika vikundi vya ushirika shuleni vinavyohusu ukulima kushiriki katika kilimo shuleni. 

Uhusiano na Maadili:                                       

uwajibikaji katika kutunza vifaa vya shambani kutunza vifaa vya shambani.

 Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: kushiriki katika ukulima nyumbani

Kuwahamasisha wengine wa rika lake kuhusu umuhimu wa kilimo.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuhakiki matamshi ya sauti mbili zinazotamkwa pamoja
  • kuchunguza anavyotumia msamiati wa shambani katika mawasiliano
  • kuchunguza anavyotumia nafsi ya tatu wakati ujao katika mawasiliano • kuchanganua anavyojibu maswali ya kusema na ya kuandika
  • kufuatilia mwandiko wake.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

Kuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti lengwa kwa ufasaha
  • anasimulia shughuli zinazofanyika shambani kwa ubunifu
  • anasoma hadithi kwa ufasaha na ukakamavu
  • anafahamu kwa urahisi hadithi aliyosoma na kusomewa
  • anaandika kisa kifupi kwa hati nadhifu na ubunifu
  • anatunga sentensi sahihi akizingatia nafsi ya tatu wakati ujao katika umoja na wingi kila wakati.

Kufikia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti ipasavyo
  • anasimulia shughuli zinazofanyika shambani
  • anasoma hadithi kwa ufasaha.
  • anafahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
  • anaandika kisa kifupi kwa hati bora
  • anatunga sentensi sahihi akizingatia nafsi ya tatu wakati ujao katika umoja na wingi.

Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka baadhi ya sauti ipasavyo
  • anasimulia baadhi ya shughuli za shambani
  • anasoma hadithi kwa ufasaha
  • ana chamgamoto katika kufahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
  • anajaribu kuandika kisa kwa hati inayosomeka
  • ana changamoto katika kutunga sentensi sahihi akizingatia nafsi ya tatu wakati ujao katika umoja na wingi.

Mbali na Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika kutamka sauti alizofunzwa 
  • ana changamoto katika kusimulia shughuli za shambani
  • ana changamoto katika kusoma hadithi  
  • ana chamgamoto katika kufahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
  • ana changamoto katika kuandika kisa
  • ana changamoto katika kutunga sentensi sahihi akizingatia nafsi ya tatu wakati ujao katika umoja na wingi

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *