MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA
Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-
- kutambua sauti mbili zinazotamkwa pamoja ili kuimarisha matamshi bora,
- kutamka sauti lengwa ili kuimarisha matamshi bora,
- kusoma silabi za sauti lengwa ili kuimarisha usomaji,
- kuandika silabi zinazotokana na sauti lengwa ili kuimarisha uandishi bora,
- kusoma maneno kwa kutumia silabi zinazotokana na sauti
lengwa ili kuimarisha usomaji,
- kuandika maneno kutokana na silabi zilizofunzwa ili kuimarisha uandishi bora,
- kusoma hadithi zilizo na maneno yaliyo na sauti lengwa ili kumsaidia mwanafunzi kutamka sauti husika na kuimarisha matamshi na usomaji,
- kuchangamkia kutamka sauti lengwa ili kuimarisha mawasiliano.
MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI
- Mwanafunzi atambue sauti mw, nd na pw katika maneno.
- Mwanafunzi asikilize mwalimu akizitamka silabi zinazotokana na sauti lengwa kisha atamke pamoja na mwalimu na baadaye atamke akiwa pekee, wawili wawili na darasa zima k.m mwa, mwe, mwi na mwo.
- Mwanafunzi aweza kutumia teknolojia kama vile papaya, tarakilishi, projekta na kipasasauti kumsaidia kuimarisha matamshi yake.
- Mwanafunzi aweza kumsikiliza mgeni mwalikwa akitamka sauti lengwa.
- Mwanafunzi atambue sauti alizosoma katika maneno kwa mfano k. m mwana, mwananchi, ndoo, ndizi, uzalendo, pwani, pweza na pweke.
- Mwanafunzi asome maneno kwa kutumia silabi na kugawa yaliyo marefu zaidi katika sehemu ndogo ndogo.
- Wanafunzi wasome hadithi zilizo na maneno yaliyobeba sauti lengwa darasani au wawili wawili.
- Mwanafunzi anakili herufi na maneno yanayotokana na sauti alizofunzwa.
- Mwanafunzi aandike maneno yanayojumuisha sauti lengwa.
- Mwanafunzi asikilize imla ya maneno yaliyo na herufi za sauti lengwa na kuyaandika.
MASWALI DADISI
- Ni sauti zipi unazojua kutamka?
- Unajua kusoma
silabi zipi katika maneno?
- Ni herufi na maneno yapi yanayoundwa kutokana na sauti mbili zinazotamkwa pamoja?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:
uraia: uzalendo – kushiriki katika kuimba wimbo wa taifa mawasiliano na ushirikiano – kushirikiana pamoja darasani kufikiri kwa kina na kutatua matatizo – Katika kujibu maswali ya ufahamu yasiyo na majibu ya moja kwa moja ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza.
Uhusiano na masuala mtambuko:
uraia: uzalendo – kushiriki katika kuimba wimbo wa taifa.
Uhusiano na masomo mengine: Environmental Activities na Movement and Creative Activities.
Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:
kushiriki katika uskauti shuleni kupandisha bendera shuleni kushiriki katika kuimba wimbo wa taifa kuimba na kukariri mashairi kuhusu uzalendo.
Uhusiano na Maadili:
umoja, uzalendo, haki za kijamii, uwajibikaji, mapenzi kwa nchi, heshima na amani.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: kushiriki katika kuimba nyimbo zinazokuza uzalendo katika sherehe mbalimbali.
Mapendekezo ya Tathmini:
- kuhakiki matamshi ya sauti mbili zinazotamkwa pamoja
- kuchunguza anavyotumia msamiati wa shambani katika mawasiliano
- kuchunguza anavyotumia –ake na -ao katika mawasiliano
- kuchanganua anavyojibu maswali ya kusema na ya kuandika
- kufuatilia mwandiko wake
- kuchunguza anavyotumia lugha katika masimulizi.
Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini
Kuzidisha Matarajio
Mwanafunzi,
- anatamka sauti ipasavyo na kwa ufasaha
- anasimulia visa vinavyohusiana na uzalendo kwa ubunifu
- anasoma hadithi kwa ufasaha na ukakamavu
- anafahamu kwa wepesi hadithi aliyosoma na kusomewa
- anatunga sentensi sahihi akitumia – ake na -ao kila wakati
- anaandika kisa kifupi kwa hati nadhifu, ubunifu, mtiririko mwafaka na kwa haraka.
Kufikia Matarajio
Mwanafunzi,
- anatamka sauti ipasavyo
- anasimulia visa vinavyohusiana na uzalendo
- anasoma hadithi kwa ufasaha
- anafahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
- anatunga sentensi sahihi akitumia –ake na -ao
- anaandika kisa kifupi kwa hati bora na kwa mtiririko ufaao.
Kukaribia Matarajio
Mwanafunzi,
- anatamka baadhi ya sauti ipasavyo
- anasimulia visa vinavyohusiana na uzalendo.
- anasoma hadithi
- anafahamu baadhi ya hadithi aliyosoma na kusomewa
- ana changamoto katika kutunga sentensi sahihi akitumia –ake na -ao
- anajaribu kuandika kisa kifupi kwa hati zinazosomeka.
Mbali na Matarajio
Mwanafunzi,
- ana changamoto katika kutamka sauti ipasavyo
- ana changamoto katika kusimulia visa vinavyohusiana na uzalendo
- ana changamoto katika kusoma hadithi
- ana changamoto katika kufahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
- ana changamoto katika kutunga sentensi sahihi akitumia –ake na -ao
- ana changamoto katika kuandika kisa.