MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA
Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-
- kusikiliza hadithi ikisomwa na mwalimu inayojumuisha miezi ili kuimarisha stadi za kusikiliza na kusoma,
- kusoma hadithi zinazojumuisha miezi na nambari ili kuimarisha usomaji,
- kufahamu hadithi aliyoisoma na aliyosomewa kuhusu miezi ya mwaka ili kupata ujumbe,
- kuchangamkia kusoma hadithi katika maisha ya kila siku.
MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI
- Mwanafunzi asikilize mwalimu akisoma hadithi.
- Mwanafunzi asome hadithi peke yake.
- Wanafunzi wasomeane hadithi wakiwa wawili wawili au katika vikundi.
- Mwanafunzi aweza kutazama video ambapo hadithi inasomwa.
- Mwanafunzi aweza kusoma hadithi kwa kutumia jitabu lililowekwa mbele ya darasa.
- Mwanafunzi ajibu na kuuliza maswali kuhusu hadithi aliyosoma.
- Mwanafunzi atoe muhtasari wa hadithi aliyosoma au kusomewa.
MASWALI DADISI
- Je, ni hadithi gani uliofurahia ukisomewa?
- Je, waweza kukumbuka nini ulichosoma au kusomewa?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:
mawasiliano na ushirikiano – kushirikiana pamoja darasani ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza.
Uhusiano na masuala mtambuko:
elimu ya kudumisha maendeleo: elimu ya maswala ya fedha: kujua kuratibu shughuli za kila siku.
Uhusiano na masomo mengine:
Mathematics Activities, Environmental Activities na English Activities
Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji: kuzingatia ratiba ya shule inayoonyesha shughuli za miezi mbalimbali
Nyimbo na mashairi kuhusu miezi ya mwaka.
Uhusiano na Maadili:
uwajibikaji uzalendo (katika kukumbuka miezi na siku za sherehe za kitaifa).
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: kushiriki katika kuratibu shughuli zinazoendeshwa katika jamii.
Mapendekezo ya Tathmini:
- kuhakiki matamshi ya sauti mbili zinazotamkwa pamoja
- kuchunguza anavyotumia msamiati wa miezi ya mwaka na tarakimu katika mawasiliano
- kuchunguza anavyotumia alama ya kikomo katika mawasiliano
- kuchanganua anavyojibu maswali ya kusema na ya kuandika
- kufuatilia mwandiko wake
kuchunguza anavyotumia lugha katika masimulizi.
Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini
Kuzidisha Matarajio
Mwanafunzi;
- anatamka sauti kwa haraka na ipasavyo
- anasimulia hadithi zinazojumuisha miezi ya mwaka kwa ubunifu
- anasoma hadithi kwa ufasaha na ukakamavu
- anafahamu kwa wepesi hadithi aliyosoma na kusomewa
- anaandika sentensi akitumia kikomo kila siku
- anaandika kisa kwa ubunifu, mtiririko na hati nadhifu na kwa haraka.
Kufikia Matarajio
Mwanafunzi;
- anatamka sauti ipasavyo
- anasimulia hadithi zinazojumuisha miezi ya mwaka
- anasoma hadithi kwa ufasaha
- anafahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
- anaandika sentensi akitumia kikomo
- anaandika kisa kwa mtiririko na hati bora.
Kukaribia Matarajio
Mwanafunzi;
- anatamka baadhi ya sauti ipasavyo
- anasimulia baadhi ya hadithi zinazojumuisha miezi ya mwaka
- anasoma hadithi
- anafahamu baadhi ya hadithi aliyosoma na kusomewa
- anaandika baadhi ya sentensi akitumia kikomo
- anaandika kisa kwa hati zinazosomeka.
Mbali na Matarajio
Mwanafunzi;
- anatamka baadhi ya sauti
- ana changamoto katika kusimulia hadithi zinazojumuisha miezi ya mwaka
- anasoma baadhi ya hadithi japo bila ufasaha ufaao
- ana changamoto katika kufahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
- ana changamoto katika kuandika sentensi akitumia kikomo
- ana changamoto katika kuandika kisa.