MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA
Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-
- kutambua msamiati uliotumiwa katika hadithi aliyosoma au kusomewa ili kuimarisha ufahamu,
- kusoma hadithi zinazohusu ndege wa nyumbani ili kujenga usomaji bora,
- kusikiliza hadithi zinazohusu ndege wa nyumbani zikisomwa ili kujenga usikivu,
- kufahamu hadithi aliyoisoma na aliyosomewa kuhusu ndege wanaofugwa ili kupata ujumbe,
- kuchangamkia kusoma hadithi ili kuendeleza ari ya kusoma zaidi.
MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI
- Mwanafunzi ajadili picha zilizojumuishwa kwenye hadithi.
- Mwanafunzi atabiri kitakachotokea kwenye hadithi.
- Mwanafunzi athibitishe utabiri wao baada ya kusoma hadithi.
- Mwanafunzi ashiriki katika kusoma darasani, wakiwa wawili na baadaye asome peke yake.
- Mwanafunzi aweza kusikiliza hadithi ya mwalimu au hadithi iliyorekodiwa.
- Wanafunzi waweza kusomeana hadithi wakiwa wawili wawili au katika vikundi.
- Wanafunzi waweza kusoma hadithi kwa kutumia vifaa vya kiteknolojia k.v. tarakilishi na projekta.
- Mwanafunzi atunge sentensi akitumia msamiati uliotumiwa katika hadithi.
- Mwanafunzi anakili majina na sentensi zinazojumuisha majina ndege wa nyumbani.
- Mwanafunzi aweza kusoma hadithi kwa kutumia jitabu lililowekwa mbele ya darasa.
- Mwanafunzi ajibu na kuuliza maswali kutokana na hadithi.
MASWALI DADISI
- Ni nini unachokiona katika picha?
- Unafikiri ni nini kitakachotokea katika hadithi?
- Unakumbuka nini kutokana na hadithi uliyosoma?
- Ni kwa nini unampenda ndege wako?
Umilisi wa kimsingi unaokuzwa: mawisiliano na ushirikiano – wanafunzi washiriki katika vikundi na wakiwa wawili wawili ujuzi wa kidijitali – matumizi ya teknolojia katika kujifunza hadithi, msamiati na sauti kufikiri kwa kina – kung’amua sifa za ndege ampendaye
Uhusiano na masuala mtambuko:
elimu ya maendeleo endelevu (masilahi ya wanyama – kujali na kutunza ndege)
Uhusiano na masomo mengine: Environmental Activities na English Activitites.
Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:
kushiriki katika vikundi shuleni kama vile chama cha ukulima kuimba na kukariri mashairi kuhusu ndege wa nyumbani.
Uhusiano na Maadili:
upendo kwa ndege wanaofugwa uwajibikaji katika kutunza ndege.
Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: kutunza ndege na wanyama.
Mapendekezo ya Tathmini:
- kuchunguza anavyotumia msamiati wa ndege wanaofugwa katika mawasiliano
- kuchunguza anavyotumia juu ya na chini ya katika mawasiliano
- kuchanganua anavyojibu maswali ya kusema na ya kuandika
- kuchunguza ufahamu wake wa hadithi aliyosoma au kusomewa • kuhakiki anavyosoma na kusimulia hadithi
- kufuatilia mwandiko wake.
Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini
Kuzidisha Matarajio
Mwanafunzi,
- anasikiliza na kusimulia hadithi kwa ukakamavu na ufasaha
- anasoma maneno, sentensi na hadithi kuhusu ndege ampendaye kwa wepesi na ufasaha
- anafahamu kwa wepesi hadithi aliyosoma na kusomewa
- anatumia juu ya na chini ya kutunga sentensi sahihi zenye ubunifu wa hali ya juu
- anaandika kisa kwa ubunifu, mtiririko, hati nadhifu na kwa haraka.
Kufikia Matarajio
Mwanafunzi,
- anasikiliza na kusimulia hadithi kwa ufasaha
- anasoma maneno, sentensi na hadithi kuhusu ndege ampendaye kwa ufasaha
- anafahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
- anatumia juu ya na chini ya kutunga sentensi sahihi
- anaandika kisa kwa
mtiririko na hati bora.
Kukaribia Matarajio
Mwanafunzi,
- anasikiliza na kusimulia hadithi
- anasoma maneno, sentensi na hadithi kuhusu ndege ampendaye
- anafahamu baadhi ya hadithi aliyosoma na kusomewa
- ana changamoto katika kutumia juu ya na chini ya kutunga sentensi sahihi
- anaandika kisa kwa hati zinazosomeka.
Mbali na Matarajio
Mwanafunzi,
- ana changamoto katika kusimulia hadithi
- ana changamoto katika kusoma baadhi ya maneno, sentensi na hadithi kuhusu ndege ampendaye
- ana changamoto katika kufahamu hadithi aliyosoma na kusomewa
- ana changamoto katika kutumia juu ya na chini ya kutunga sentensi sahihi
ana changamoto katika kuandika kisa.