Please Limited time Offer!

MATOKEO MAALUM YANAYOTARAJIWA

Kufikia mwisho wa mada, mwanafunzi aweze:-

  1. kutambua msamiati uliotumiwa katika hadithi ili kuimarisha mawasiliano,
  2. kusikiliza hadithi zikisomwa na mwalimu zinazohusu usafi wa mwili katika kujenga stadi ya kusoma,
  3. kusoma hadithi zinazohusu usafi wa mwili katika kujenga stadi ya kusoma,
  4. kufahamu hadithi aliyoisoma na aliyosomewa kuhusu usafi wa mwili ili kuimarisha mawasiliano,
  5. kudumisha usafi katika maisha ya kila siku. 

MAPENDEKEZO YA SHUGHULI ZA UJIFUNZAJI

  • Mwanafunzi ajadili picha zilizojumuishwa kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi atabiri kitakachotokea kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi athibitishe utabiri wake baada ya kusoma na kusomewa hadithi.
  • Mwanafunzi asome hadithi baada ya mwalimu, kisha pamoja na mwalimu na baadaye akiwa peke yake au wawili wawili.
  • Mwanafunzi aeleze maana na matumizi ya msamiati uliotumika kwenye hadithi.
  • Mwanafunzi asikilize mwalimu anaposoma hadithi, asome pamoja na mwalimu kisha asome peke yake. 
  • Mwanafunzi aweza kusikiliza hadithi ya mwalimu au hadithi iliyorekodiwa kuhusu usafi.
  • Wanafunzi waweza kusomeana hadithi wakiwa wawili wawili na katika vikundi.
  • Mwanafunzi aweza  kusoma hadithi kupitia  vifaa vya kiteknolojia kama vile tarakilishi, projekta n.k. 
  • Mwanafunzi asome maneno yanayohusu usafi kwenye kadi. 
  • Mwanafunzi aweza kuhusishwa katika kuigiza vitendo vinavyohusu usafi wa mwili.
  • Mwanafunzi aweza  kusoma hadithi kwa kutumia jitabu lililowekwa mbele ya darasa. 
  • Mwanafunzi aweza kuonyeshwa picha zinazoashiria vitendo vya usafi wa mwili.
  • Mwanafunzi aulize na kujibu maswali kutokana na hadithi.

MASWALI DADISI

  1. Je, ni nini maana ya usafi gani?
  2. Je, ni matayarisho yapi unayofanya kabla ya kuja shuleni?
  3. Unafikiri ni nini kitakachotokea katika hadithi hii?
  4. Je, ni hadithi gani

umewahi kusoma?

Umilisi wa kimsingi unaokuzwa:

mawasiliano na ushirikiano –  mwanafunzi anashiriki katika makundi kuimba na kukariri mashairi, kusimulia na kujadiliana  hamu ya ujifunzaji: mwanafunzi atajenga msingi wa kusoma na kutafiti zaidi kuhusu usafi ujuzi wa kidijitali : vifaa vya kiteknolojia vinatumiwa katika kusimulia, kuimba na kukariri mashairi ubunifu: mwanafunzi anajenga ubunifu wake anaposimulia na kutunga sentensi akitumia maneno ya vitendo.

Uhusiano na masuala mtambuko:  elimu ya afya –  usafi wa kibinafsi wanapozingatia usafi wa mwili wao.

Uhusiano na Masomo mengine:  

English Activities, Environmental Activities, Health and Nutrition na Religious Activities  

 Mapendekezo ya shughuli zingine zilizoratibiwa za ujifunzaji:  

kazi ya vikundi  shughuli za vikundi vya ushirika shuleni michezo nyimbo na mashairi kuhusu usafi wa mwili.

 Uhusiano na Maadili: 

uwajibikaji.  

Mapendekezo ya shughuli za huduma za kijamii zinazochangia ujifunzaji: 

kusisitiza kuhusu utunzaji wa mwili miongoni mwa wenzake kulinda usiri wa mwili wake.

Mapendekezo ya Tathmini:

  • kuuliza maswali kuhusu jinsi ya kuzingatia usafi wa mwili, 
  • kuchunguza anavyotamka sauti zilizofunzwa, 
  • kuchunguza jinsi mwanafunzi anavyojibu maswali ya masimulizi na hadithi na kutoa muhtasari wa hadithi aliyosomewa au kusimuliwa, 
  • kuchunguza jinsi anavyotumia huyu na hawa katika sentensi.

Viwango vya Kuzingatia katika Kutathmini

lKuzidisha Matarajio

Mwanafunzi,

  • anatamka sauti lengwa kwa ufasaha
  • anaelezea jinsi ya kuzingatia usafi wa mwili kwa ufasaha
  • anatumia msamiati wa usafi wa mwili kwa ubunifu katika sentensi
  • anasoma kwa ufasaha
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa ubunifu na usahihi 
  • anatumia huyu na hawa kutunga sentensi kwa ubunifu
  • anaandika kwa hati nadhifu.

Kufikia Matarajio

            Mwanafunzi,

  • anatamka sauti lengwa vyema
  • anaelezea jinsi ya kuzingatia usafi wa mwili
  • anatumia msamiati unaotumika katika usafi wa mwili ifaavyo katika sentensi.
  • anasoma ifaavyo
  • anajibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi
  • anatumia huyu na hawa kutunga sentensi ifaavyo
  • anaandika kwa hati bora.

         Kukaribia Matarajio

Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika kutamka baadhi ya sauti lengwa vyema
  • anaelezea jinsi ya kuzingatia usafi wa mwili
  • ana changamoto katika kutumia baadhi ya misamiati ya usafi wa mwili ifaavyo katika sentensi
  • anasoma baadhi ya kazi anazopewa
  • anajibu baadhi ya maswali ya ufahamu katika  hadithi na masimulizi kwa usahihi
  • ana changamoto za kutumia umoja na wingi wa majina lengwa katika kutunga sentensi 
  • anaandika kwa hati zinazosomeka.

Mbali na Matarajio

                Mwanafunzi,

  • ana changamoto katika kutamka sauti lengwa vyema
  • ana changamoto katika kuelezea jinsi ya kuzingatia usafi wa mwili
  • ana changamoto katika kutumia msamiati usafi wa mwili ifaavyo katika sentensi
  • ana changamoto katika kusoma
  • Ana changamoto katika kujibu maswali ya ufahamu katika hadithi na masimulizi kwa usahihi 
  • ana changamoto katika kutumia umoja na wingi wa majina lengwa katika kutunga sentensi
  • ana changamoto katika  kuandika.

This is paragraph 2 for posts without the target word.

By Depa

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *